5 Katika muji ule wakamukuta mufalme Adoni-Bezeki, wakapigana naye na kuwashinda Wakanana na Waperizi.
Basi, kukatokea ugomvi kati ya wachungaji wa Abramu na wachungaji wa Loti. Wakati ule, Wakanana na Waperizi ndio waliokuwa wenyeji wa inchi hiyo.
Basi watu wa kabila la Yuda wakaenda kufanya mashambulio, naye Yawe akawatia Wakanana na Waperizi katika mikono yao, wakawaua watu elfu kumi katika vita kule Bezeki.
Adoni-Bezeki akakimbia, lakini walimufuatilia, wakamukamata, wakamukata vidole gumba vya mikono na miguu.
Basi, Waisraeli waliishi pamoja na Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
Saulo alipowapanga Waisraeli kule Bezeki akakuwa na watu elfu mia tatu kutoka inchi ya Israeli na elfu makumi tatu kutoka inchi ya Yuda.