Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Waamuzi 1:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Yawe akawajibu: “Kabila la Yuda litakwenda kupigana nao kwanza, maana nimeitia inchi hiyo katika mikono yao.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Waamuzi 1:2
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wale watakaopiga kambi upande wa mashariki watakuwa kikundi cha watu wanaokuwa chini ya bendera ya Yuda na kiongozi wao atakuwa Nasoni mwana wa Aminadabu.


Wale waliotoa sadaka ni hawa: Siku ya kwanza: Nasoni mwana wa Aminadabu, wa kabila la Yuda; Siku ya pili: Netaneli mwana wa Suari, wa kabila la Isakari; Siku ya tatu: Eliabu mwana wa Heloni, wa kabila la Zebuluni; Siku ya ine: Elisuri mwana wa Sedeuri, wa kabila la Rubeni: Siku ya tano: Selumieli mwana wa Suri-Shadai, wa kabila la Simeoni; Siku ya sita: Eliasafu mwana wa Deueli, wa kabila la Gadi; Siku ya saba: Elisama mwana wa Amihudi, wa kabila la Efuraimu; Siku ya nane: Gamalieli mwana wa Pedasuri, wa kabila la Manase; Siku ya tisa: Abidani mwana wa Gideoni, wa kabila la Benjamina; Siku ya kumi: Ahiezeri mwana wa Amishadai, wa kabila la Dani; Siku ya kumi na moja: Pagieli mwana wa Okrani, wa kabila la Aseri; Siku ya kumi na mbili: Ahira mwana wa Enani, wa kabila la Nafutali. Hii ni sadaka iliyotolewa na kila mumoja: sahani moja ya feza yenye uzito wa kilo moja na nusu na beseni moja la feza lenye uzito wa grama mia nane kulingana na vipimo vya hema takatifu; sahani na beseni hilo vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya sadaka ya vyakula; kisahani kimoja cha zahabu chenye uzito wa grama mia moja na kumi kikiwa kimejazwa ubani; mwana-ngombe dume mumoja, kondoo dume mumoja, na mwana-kondoo dume mumoja wa mwaka mumoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; beberu mumoja kwa ajili ya sadaka ya zambi; ngombe dume wawili, kondoo dume watano, beberu watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mumoja kwa ajili ya sadaka za amani.


Kwa maana inajulikana wazi kwamba Bwana wetu alitoka katika kabila la Yuda, na juu ya kabila lile Musa hakusema hata neno moja linaloelekea ukuhani.


Wakamwambia: “Hakika Yawe ameitia inchi yote katika mikono yetu. Tena wakaaji wa inchi hiyo wametetemeka kwa sababu yetu.”


Basi mumoja kati ya wale wazee akaniambia: “Usilie. Angalia, simba wa kabila la Yuda, wa uzao wa mufalme Daudi, amepata ushindi. Yeye anaweza kuvunja vile vifundo saba vya muhuri vya kizingo na kukifungua.”


Watu wa kabila la Yuda wakawaambia wandugu zao, watu wa kabila la Simeoni: “Mushirikiane nasi tunapokwenda kuitwaa inchi hiyo ambayo tumepewa. Nasi, vilevile tutashirikiana nanyi kwenda kuitwaa inchi mutakayopewa.” Hivyo kabila la Simeoni likakubali kushirikiana nao.


Waisraeli wakaenda Beteli kuomba shauri kwa Mungu, wapate kujua kabila ambalo litakwenda kwanza kupigana na watu wa kabila la Benjamina. Yawe akataja kabila la Yuda liende kwanza.


Finehasi mwana wa Eleazari mwana wa Haruni alikuwa na kazi ya kutumika mbele yake. Waisraeli wakamwuliza Yawe: “Twende tena kupigana na wandugu zetu, watu wa kabila la Benjamina?” Yawe akawaambia: “Muende. Kesho nitawatia katika mikono yenu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ