Ujumbe wa Mungu juu ya Tiro. Muomboleze, enyi mashua makubwa za kutoka Tarsisi. Kivuko na muji wenu vimeharibiwa. Mutapokea habari hizo mutakaporudia kutoka Kipuro.
Sehemu hiyo moja ya tatu itakayobaki, nitaipima na kuitakasa, kama vile mutu anavyosafisha feza, kama vile wanavyopima zahabu. Halafu wao wataniomba mimi, nami nitawajibu. Nitasema: Hawa ni watu wangu, nao watasema: Yawe, ndiye Mungu wetu.
Mukia wake ulikokota sehemu moja ya tatu ya nyota za mbingu na kuzitupa katika dunia. Yule nyoka akasimama mbele ya yule mwanamuke aliyekuwa tayari kuzaa, kusudi amumeze mutoto wakati atakapozaliwa.
Malaika wa pili akamwanga kikombe chake katika bahari. Maji yakageuka na kuwa kama damu ya mufu, na viumbe vyote vyenye uzima vilivyokuwa ndani ya bahari vikakufa.
Kisha malaika wa tatu akapiga baragumu. Halafu nyota kubwa iliyowaka kama mwenge, ikaanguka toka mbinguni na kujitupa juu ya sehemu moja ya tatu ya mito na juu ya chemichemi.
Kisha malaika wa ine akapiga baragumu. Sehemu moja ya tatu ya jua ikaharibishwa pamoja na sehemu moja ya tatu ya mwezi na ya nyota. Sehemu zile tatu zikaingiwa na giza. Hivi hakukuwa mwangaza kwa muda wa sehemu moja ya tatu ya saa za muchana na sehemu moja ya tatu ya saa za usiku vilevile.
Malaika wa kwanza akapiga baragumu. Halafu mvua ya mawe na moto vyenye kuchanganyika na damu, vikatupwa katika dunia. Sehemu moja ya tatu ya inchi ikateketea, na sehemu moja ya tatu ya miti na majani yote vikateketea vilevile.