Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ufunuo 8:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Kisha malaika mwingine akakuja kusimama karibu na mazabahu. Alikuwa akishika chetezo cha zahabu. Naye akapewa ubani mwingi kusudi autoe sadaka pamoja na maombi ya watu wote wa Mungu juu ya mazabahu ya zahabu iliyokuwa mbele ya kiti cha kifalme.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ufunuo 8:3
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Upokee maombi yangu kama ubani; ninapoinua mikono yangu kwako, unikubali kama sadaka ya magaribi.


Akaweka ile mazabahu ya zahabu katika hema, mbele ya pazia,


Basi, mumoja wa hao wamalaika akaruka na kunifikia, akiwa ameshika katika mukono koleo lililokuwa na kaa la moto alilolitwaa kwenye mazabahu.


mazabahu ya mbao. Urefu wake kwenda juu ulikuwa metre moja na nusu na upana wa metre moja. Pembe zake, tako lake, na pande zake zote zilikuwa zimetengenezwa kwa mbao. Yule mutu akaniambia hivi: Hii ndiyo meza inayokaa mbele ya Yawe.


Nilimwona Yawe akisimama pembeni ya mazabahu, naye akaniamuru: Piga zile nguzo za hekalu mpaka misingi yake itikisike. Uvunje zile nguzo ziwaangukie watu juu ya vichwa. Wale watakaobaki nitawaua kwa upanga; hakuna hata mumoja wao atakayeponyoka, hakuna atakayetoroka.


Watu wa mataifa katika dunia yote tokea upande jua linapopanda mpaka upande jua linaposhuka wanalitukuza jina langu. Kila pahali wananifukizia ubani na kunitolea sadaka zinazokubaliwa; maana jina langu linatukuzwa kati yao.


Halafu watatandaza kitambaa cha rangi ya samawi juu ya mazabahu ya zahabu na kuifunika kwa ngozi laini ya mbuzi. Halafu wataingiza miti yake ya kuibebea.


Kundi kubwa la watu walikuwa inje wakiomba saa ile Zakaria alipokuwa akichoma ubani.


Ni nani anayeweza basi kuwahukumu? Hakuna hata mumoja! Maana Yesu Kristo ndiye aliyekufa, na zaidi ya hiyo, alifufuka, na sasa anakaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu, na yeye ndiye anayetuombea.


Ni kwa sababu hii anaweza kuwaokoa kabisa wao wanaokuja kwa Mungu kwa njia yake, kwa maana yeye anaishi siku zote kusudi akuwe mwombezi mbele ya Mungu.


Ndani ya chumba kile kulikuwa chombo cha kufukizia ubani, kilichotengenezwa na zahabu. Na kulikuwa vilevile Sanduku la Agano lililopakaliwa zahabu pande zote. Ndani ya sanduku lile kulikuwa kopo la zahabu lenye mana, na fimbo ya Haruni iliyoota vichipukizi juu yake. Kulikuwa vilevile vibao vya mawe vyenye Maandiko ya Agano la Mungu.


Kisha nikaona malaika mwingine mwenye uwezo akishuka toka mbinguni. Alikuwa akifunikwa na wingu, naye alikuwa na upindi wa mvua juu ya kichwa chake. Uso wake ulingaa kama jua na miguu yake ilimetameta kama nguzo ya ndimi za moto.


Kisha kukatokea malaika mwingine mwenye uwezo wa kuamuru moto, akatoka kwenye mazabahu, akamwambia kwa sauti kubwa yule aliyekuwa na kisu kikali cha kuvuna: “Nyoosha kisu chako, ukate matunda ya mizabibu yanayokuwa katika dunia kwa maana zabibu zimekomaa.”


Wakati alipokuwa amekwisha kukamata kizingo, vile viumbe vine vya ajabu na wale wazee makumi mbili na wane wakainama uso mpaka chini mbele ya Mwana-Kondoo. Kila mumoja wao alikuwa na kinubi na vikombe vya zahabu vilivyojaa marasi, ndiyo maombi ya watu wa Mungu.


Wakati Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa tano, nikaona chini ya mazabahu, roho za watu waliouawa kwa sababu ya kutangaza Neno la Mungu na kwa sababu ya ushuhuda wao.


Nikaona malaika mwingine akipanda tokea mashariki alikuwa akishika muhuri wa Mungu Mwenye Uzima. Akawalalamikia kwa sauti kubwa wale wamalaika wane waliopewa uwezo wa kuharibu dunia na bahari:


Moshi wa ule ubani pamoja na maombi ya watakatifu vilipanda mbele ya Mungu toka katika mukono wa yule malaika.


Kisha yule malaika akatwaa kile chetezo, akakijaza makaa ya moto toka kwenye mazabahu na kukitupa katika dunia. Na halafu kukakuwa ngurumo ya radi, makelele, umeme na tetemeko la inchi.


Malaika wa sita akapiga baragumu. Halafu nikasikia sauti moja ikitokea kwenye pembe ine za mazabahu ya zahabu iliyokuwa mbele ya Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ