Kweli, nitawashambulia wale waliowakamata mateka, nao watakamatwa mateka na wale waliowafanya watumwa wao. Halafu kwa hiyo mutajua kwamba Yawe wa majeshi ndiye aliyenituma.
Kisha nikaona kizingo cha karatasi katika mukono wa kuume wa yule aliyeikaa juu ya kiti cha kifalme. Kizingo kile kilikuwa kimeandikwa ngambo na ngambo na kufungwa kwa vifundo saba vya mihuri.
Nao walikuwa wakiimba wimbo huu mupya wakisema: “Wewe unastahili kukamata kizingo cha karatasi, na kuvunja vifundo vya mihuri yake. Kwa sababu wewe uliuawa, na kwa njia ya damu yako, ulikomboa kwa ajili ya Mungu watu wa kila kabila, wa kila luga, wa kila jamaa na wa kila taifa.
Kisha nikaona mambo haya: Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa kwanza kati ya ile mihuri saba, nikasikia kimoja kati ya vile viumbe vya ajabu kikisema hivi kwa sauti kama ya ngurumo ya radi: “Kuja!”
Kisha nikaona mambo haya: Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa sita, kukakuwa tetemeko kubwa la dunia; jua ikageuka kuwa nyeusi kama nguo ya kilio na mwezi ukageuka kuwa mwekundu kama damu.
Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa tatu, nikasikia kiumbe cha tatu cha ajabu kikisema: “Kuja!” Niliangalia nami nikaona farasi mweusi. Na yule aliyepanda juu yake alikuwa na mizani katika mikono yake.
Wakati Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa tano, nikaona chini ya mazabahu, roho za watu waliouawa kwa sababu ya kutangaza Neno la Mungu na kwa sababu ya ushuhuda wao.