Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ufunuo 6:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Niliangalia, nami nikaona farasi mumoja mweupe. Na yule aliyepanda juu yake alikuwa na upindi, akapewa taji. Akatoka akiwa mushindaji na mwenye uwezo wa kuendelea kushinda.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ufunuo 6:2
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe ataeneza mamlaka yako kutoka Sayuni; utatawala juu ya waadui zako wote.


Ulipowakaripia, ee Mungu wa Yakobo, farasi na wapanda-farasi walipooza.


Zaburi. Mumwimbie Yawe wimbo mupya, kwa maana ametenda mambo ya ajabu! Nguvu yake kubwa, mukono wake mutakatifu umemupatia ushindi.


Bwana wetu Yawe atakiangamiza kifo milele! Atayafuta machozi katika nyuso za watu wote na kuondoa haya ya watu wake katika dunia yote. Yawe amesema hivyo.


Wakati wa usiku, nilimwona malaika akipanda juu ya farasi mwekundu. Malaika yule alikuwa akisimama katika bonde, katikati ya miti ya mihadasi. Nyuma yake kulikuwa farasi wengine wekundu, wa kijivujivu na weupe.


Kisha Yesu akakuja karibu nao, na kuwaambia: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na katika dunia.


Kwa maana Kristo anapaswa kutawala mpaka atakapowashinda waadui zake wote na kuwaweka chini ya miguu yake.


Kisha malaika wa saba akapiga baragumu. Halafu sauti kubwa zikasikilika katika mbingu, zikisema: “Sasa utawala juu ya dunia ni wa Bwana wetu na wa Masiya wake. Naye atatawala kwa milele na milele!”


Watu wa mataifa mengine walikasirika, lakini kasirani yako imetokea. Sasa ni wakati wa kuhukumu waliokufa, nao wakati wa kuwapa waliokutumikia zawadi, ndio manabii wako, na wote wanaoheshimu jina lako, wakubwa na wadogo. Ni wakati wa kuangamiza wale wanaoharibu dunia!”


Niliangalia tena, nami nikaona wingu jeupe, na juu ya wingu lile kulikuwa kukiikaa kiumbe kimoja kinachofanana na Mwana wa Mutu. Juu ya kichwa chake kulikuwa taji la zahabu, naye alikuwa akishika kisu kikali cha kuvuna katika mukono wake.


Tena nikaona kitu kinachofanana na bahari ya kioo, iliyochanganyika na moto. Nikaona vilevile wale walioshinda yule nyama wa ajabu pamoja na sanamu yake na tarakimu zinazolingana na herufi za jina lake. Watu wale walikuwa wakisimama juu ya ile bahari ya kioo wakishika vinubi walivyopewa na Mungu.


Watapigana vita na Mwana-Kondoo, lakini Mwana-Kondoo pamoja na waaminifu wake aliowaita na kujichagulia atawashinda, kwa sababu yeye ni Bwana wa wabwana na Mufalme wa wafalme.”


Makundi ya wakaaji wa mbinguni wakamufuata, nao walikuwa wakipanda juu ya farasi weupe na kuvaa nguo safi nyeupe za kitani.


Yule atakayeshinda, nitamwikalisha karibu nami kwenye kiti changu cha kifalme, kama vile mimi nilivyoshinda na kuikaa karibu na Baba yangu kwenye kiti chake cha kifalme.


Umbo la nzige wale lilifanana na farasi waliopambwa kwa kupigana vita. Juu ya vichwa vyao kulikuwa vitu vinavyofanana na taji za zahabu, na nyuso zao zilifanana kama nyuso za watu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ