Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ufunuo 4:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kiumbe cha kwanza kilifanana na simba, kiumbe cha pili kilifanana na mwana-ngombe na kiumbe cha tatu kilifanana na mutu na kiumbe cha ine kilifanana na tai anayeruka.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ufunuo 4:7
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wewe Yuda, mwana wangu, ni kama mwana-simba ambaye amepata mawindo yake akapanda juu, kama simba mukali anajinyoosha na kulala chini. Simba dike, nani anayesubutu kumwamusha?


Saulo na Yonatani, watu wema na wa kupendeza. Katika maisha na kifo hawakutengana. Walikuwa wepesi kuliko tai, wenye nguvu kuliko simba.


Taifa lenye fujo lina viongozi wengi, lakini kwa kiongozi mumoja mwenye akili na maarifa kuna utengemano.


Lakini wote wanaomutumainia Yawe, watapata nguvu mupya. Watapanda juu kwa mabawa kama tai, watakimbia bila kuchoka, watatembea bila kuregea.


Juu ya nyuso zao: kila kimoja kilikuwa na uso wa mutu upande wa mbele, uso wa simba upande wa kuume, uso wa ngombe upande wa kushoto, na uso wa tai upande wa nyuma.


Chini ya mabawa yao, kulikuwa mikono inayokuwa sawa ya mutu. Mikono hiyo ilikuwa inaelekea kwenye pande zote ine pamoja na nyuso zao na mabawa yao.


Kila kerubi alikuwa na nyuso ine: uso wa kwanza ulikuwa wa kerubi, uso wa pili ulikuwa wa mwanadamu, uso wa tatu ulikuwa wa simba na uso wa ine ulikuwa wa tai.


Kila mumoja wao alikuwa na nyuso ine na mabawa mane na chini ya kila bawa kulikuwa kitu kinachokuwa kama mukono wa mutu.


Nyama wa kwanza alikuwa kama simba, na alikuwa na mabawa kama ya tai. Nikiwa ninamwangalia, mabawa yake yaliongolewa, naye akainuliwa na kusimama kwa miguu miwili kama mutu. Kisha, akapewa akili ya kimutu.


Hata ukiruka juu kama tai, ukifanya makao yako kati ya nyota, mimi nitakushusha chini tu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Angalia! Waisraeli wameinuka kama simba dike, wanasimama kama simba dume. Ni kama simba asiyelala mpaka amalize windo lake, na kunywa damu ya windo.


Atavizia na kulala chini kama simba, nani atasubutu kumwamusha? Abarikiwe yeyote atakayekubariki wewe Israeli, alaaniwe yeyote atakayekulaani.


Wandugu zangu, musikuwe kama watoto kwa kufikiri: lakini katika mambo mabaya, iwatokee kutenda kama watoto wachanga. Inafaa mafikiri yenu yakuwe kama ya watu wazima.


“Yawe ataleta kutoka mbali taifa moja liwashambulie mbio kama tai, taifa ambalo hamujui luga yake.


Tena mbele ya kiti kile kulionekana kama bahari ya kioo, kulingaa sana kama kilauri. Kile kiti cha kifalme kilikuwa kimezungukwa pande zote na viumbe vine vya ajabu, vyenye kujaa macho mbele na nyuma.


Kisha Mwana-Kondoo akafungua kifundo cha muhuri wa pili. Nikasikia kiumbe cha pili cha ajabu kikisema: “Kuja!”


Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa tatu, nikasikia kiumbe cha tatu cha ajabu kikisema: “Kuja!” Niliangalia nami nikaona farasi mweusi. Na yule aliyepanda juu yake alikuwa na mizani katika mikono yake.


Wakati Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa ine, nikasikia sauti ya kiumbe cha ine cha ajabu kikisema: “Kuja!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ