Ufunuo 4:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20024 Na kiti kile kilikuwa kimezungukwa na viti vingine makumi mbili na vine vya kifalme na juu ya viti vile kulikuwa kumeikaa wazee makumi mbili na wane. Wale wazee walikuwa wamevaa nguo nyeupe na juu ya kichwa chao kulikuwa taji za zahabu. အခန်းကိုကြည့်ပါ။ |
Kisha nikaona viti vya kifalme na watu waliokuwa wakiikaa juu yao, wakapewa uwezo wa kuhukumu. Nikaona vilevile roho za wale waliochinjwa kwa sababu ya kutangaza ukweli ulioshuhudiwa na Yesu na Neno la Mungu. Watu wale hawakumwabudu yule nyama wa ajabu, wala sanamu yake, wala hawakupigwa chapa yake juu ya paji za nyuso zao, au juu ya mikono yao. Nao wakafufuka na kutawala pamoja na Kristo muda wa miaka elfu moja.
Kisha mambo haya, nikaangalia nami nikaona mukutano mukubwa sana wa watu wasioweza kuhesabiwa. Kulikuwa watu wa kila taifa, wa kila kabila, wa kila jamaa na wa kila luga. Walikuwa wakisimama mbele ya kiti cha kifalme na mbele ya Mwana-Kondoo, wakivaa kanzu nyeupe na kushika matawi ya muti wa ngazi katika mikono yao.