Ufunuo 4:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
3 Mutu yule aliangaa kama mawe ya bei kali ya yaspi na sardio. Kiti kile cha kifalme kilikuwa kimezungukwa na upindi wa mvua uliongaa kama jiwe la zumaridi.
Katika mwaka mufalme Uzia alipokufa, nilimwona Bwana katika maono akiikaa katika kiti cha kifalme kinachoinuka juu sana. Pindo la nguo yake lilienea katika hekalu lote,
Juu ya kitu hicho niliona kitu kimoja kinachofanana na kiti cha kifalme chenye rangi la jiwe la yakuti. Juu yake kulikuwa kunaikaa kitu kinachofanana na mutu.
Ulionekana kama upindi wa mvua wakati wa mvua. Ulionekana kufanana na utukufu wa Yawe. Nilipouona, nilianguka uso mpaka chini, nikasikia sauti ya mutu mwenye kusema.
Kisha nikaona kwamba katika lile anga juu ya vichwa vya makerubi kulikuwa kitu kinachofanana na jiwe la rangi ya samawi, umbo lake kama kiti cha kifalme.
Ulikaa Edeni, bustani ya Mungu. Ulipambwa kwa kila namna ya mawe ya bei kali, akiki, topazi, yaspi, zabarajadi, berili, sardoniki, yakuti samawi, almasi na zumaridi. Ulikuwa na mapambo ya zahabu. Yote uliwekewa tayari siku ulipoumbwa.
Kisha nikaona malaika mwingine mwenye uwezo akishuka toka mbinguni. Alikuwa akifunikwa na wingu, naye alikuwa na upindi wa mvua juu ya kichwa chake. Uso wake ulingaa kama jua na miguu yake ilimetameta kama nguzo ya ndimi za moto.