Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ufunuo 4:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Na mara moja nikashikwa na Roho wa Mungu. Nikaona kiti cha kifalme kimewekwa kule mbinguni na mutu mumoja alikuwa akiikaa juu ya kiti kile.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ufunuo 4:2
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Mikaya akasema: “Sasa sikia neno la Yawe: Nilimwona Yawe akiikaa katika kiti chake cha kifalme, na jeshi lote la mbinguni likisimama pembeni yake, upande wake wa kuume na wa kushoto.


Yawe yuko katika hekalu lake takatifu; kiti cha kifalme cha Yawe kiko mbinguni. Kwa macho yake anawachungulia wanadamu, na kujua kila kitu wanachofanya.


Katika mwaka mufalme Uzia alipokufa, nilimwona Bwana katika maono akiikaa katika kiti cha kifalme kinachoinuka juu sana. Pindo la nguo yake lilienea katika hekalu lote,


Kuna kiti cha kifalme chenye utukufu kinachoinuka juu tangu mwanzo wa vyote, ndipo pahali petu patakatifu.


Juu ya kitu hicho niliona kitu kimoja kinachofanana na kiti cha kifalme chenye rangi la jiwe la yakuti. Juu yake kulikuwa kunaikaa kitu kinachofanana na mutu.


Ulionekana kama upindi wa mvua wakati wa mvua. Ulionekana kufanana na utukufu wa Yawe. Nilipouona, nilianguka uso mpaka chini, nikasikia sauti ya mutu mwenye kusema.


Kisha nikaona kwamba katika lile anga juu ya vichwa vya makerubi kulikuwa kitu kinachofanana na jiwe la rangi ya samawi, umbo lake kama kiti cha kifalme.


Nilipokuwa nikiendelea kuangalia, nikaona viti vya kifalme viliwekwa hapo, kisha Muzee mumoja wa zamani sana akakuja, akaikaa. Alikuwa amevaa nguo nyeupe kama teluji; nywele zake zilikuwa kama sufu safi. Kiti chake cha kifalme kilikuwa ndimi za moto, na magurudumu ya kiti kile yalikuwa moto unaowaka.


Na Yesu akawaambia: “Basi namna gani Daudi, akiongozwa na Roho, aliweza kumwita ‘Bwana’, akisema:


Jambo la lazima sana katika maneno tunayosema sasa ni hili. Tuko na Mukubwa wa namna ile, anayeikaa na mamlaka katika mbingu kwa kuume kwa Mwenyezi Mungu.


Siku moja ya kumwabudu Bwana, nikashikwa na Roho wa Mungu, nikasikia sauti kubwa, inayolia kama baragumu,


Halafu yule mwanamuke akazaa mutoto mwanaume atakayetawala mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Lakini mutoto yule akanyanyuliwa na kupelekwa kwa Mungu kwenye kiti chake cha kifalme.


Nikashikwa na Roho wa Mungu, na malaika akanipeleka katika jangwa. Kule nikaona mwanamuke aliyekuwa akiikaa juu ya nyama mumoja wa ajabu mwekundu aliyeandikwa juu yake majina ya kumutukana Mungu. Nyama yule alikuwa na vichwa saba na pembe kumi.


Na wale wazee makumi mbili na wane na vile viumbe vine vya ajabu wakainama chini na kumwabudu Mungu, anayeikaa juu ya kiti cha kifalme, wakisema: “Amina! Mungu asifiwe!”


Kisha nikaona kiti kikubwa cheupe cha kifalme pamoja na yule aliyeikaa juu yake. Dunia na mbingu vikatoweka mbele yake navyo havikuonekana tena.


Nikashikwa na Roho, na malaika akanipeleka juu ya mulima mukubwa na murefu. Akanionyesha muji mutakatifu, ndio Yerusalema uliokuwa ukishuka toka mbinguni kwa Mungu,


Basi yule aliyekuwa akiikaa juu ya kiti cha kifalme akasema: “Angalia ninafanya vitu vyote kuwa vipya.” Kisha akaniambia: “Andika maneno haya, kwa maana ni ya kweli na ya uhakika.”


Yule atakayeshinda, nitamwikalisha karibu nami kwenye kiti changu cha kifalme, kama vile mimi nilivyoshinda na kuikaa karibu na Baba yangu kwenye kiti chake cha kifalme.


wale wazee makumi mbili na wane waliinama uso mpaka chini mbele ya yule anayeikaa juu ya kiti cha kifalme, wakimwabudu huyo anayeishi kwa milele na milele. Nao walikuwa wakikuja kuweka taji zao mbele ya kiti chake, na kusema:


Umeme ulipiga tokea katika kiti kile, na makelele na ngurumo ya radi vilisikilika. Mbele ya kiti kile kulikuwa kukiwaka mienge saba, na hizo ndizo zile roho saba za Mungu.


Vile viumbe vine vya ajabu viliimba kwa kumutukuza, kumuheshimia na kumushukuru yule aliyeikaa juu ya kiti cha kifalme, yule anayeishi kwa milele na milele. Kila mara vilipofanya vile,


Kisha nikaona kizingo cha karatasi katika mukono wa kuume wa yule aliyeikaa juu ya kiti cha kifalme. Kizingo kile kilikuwa kimeandikwa ngambo na ngambo na kufungwa kwa vifundo saba vya mihuri.


Nikasikia vilevile viumbe vyote vinavyokuwa mbinguni, katika dunia, katika kuzimu na vile vinavyokuwa katika bahari; viumbe vyote vya ulimwengu nzima vikimwimbia: “Utukufu, heshima, sifa na nguvu milele na milele, kwa yule anayeikaa juu kiti cha kifalme na kwa Mwana-Kondoo.”


Nao wakaiambia milima na mawe: “Mutuangukie na kutufunika mbali na yule anayeikaa juu ya kiti cha kifalme na mbali na kasirani ya Mwana-Kondoo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ