Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ufunuo 4:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Nyuma ya mambo hayo nilipata maono mengine. Niliona mulango mumoja umefunguliwa wazi mbinguni. Halafu ile sauti niliyosikia mara ya kwanza, iliyolia kama baragumu, ikaniambia: “Panda huku, nami nitakuonyesha mambo yanayopaswa kutokea nyuma ya hayo ya mbele.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ufunuo 4:1
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli ambao walikwenda Misri, kila mumoja na jamaa yake:


Yawe akasema: “Teremuka chini kisha urudi pamoja na Haruni. Lakini usiwaruhusu makuhani na watu wengine wapite mupaka na kuja kwangu, kama sivyo nitawaazibu.”


Yawe akamwambia Musa: Kuja kwangu juu kwenye mulima, ungoje kule. Mimi nitakupa vibao vya mawe vyenye sheria na amri nilizoandika kwa ajili ya kuwafundisha Waisraeli.


maana ni heri kuambiwa: “Kuja huku mbele”, kuliko kuporomoshwa mbele ya mukubwa.


Kwa siku ya tano ya mwezi wa ine, mwaka wa makumi tatu, wakati nilipokuwa katikati ya wale watu waliopelekwa katika uhamisho, karibu na muto Kebari, mbingu zikafunguka, nikapata maono toka kwa Mungu.


Yesu alipokwisha kubatizwa na kutoka ndani ya maji, mara moja mbingu zikafunguka, naye akamwona Roho wa Mungu akishuka kwa mufano wa njiwa na kukaa juu yake.


Mara moja wakati Yesu alipotoka ndani ya maji, akaona mbingu zinafunguka na Roho Mutakatifu akishuka juu yake kwa mufano wa njiwa.


Watu wale wote walipobatizwa, Yesu akabatizwa vilevile. Alipokuwa akiomba, mbingu zikafunguka,


Lakini wakati yule Roho wa ukweli atakapokuja, atawaongoza ninyi kufuata ukweli wote kabisa. Yeye hatasema kwa mamlaka yake mwenyewe, lakini atasema tu yale atakayosikia, naye atawatangazia ninyi habari za mambo yatakayokuja.


Akaona katika maono mbingu imefunguliwa wazi, na kitu kimoja kinachokuwa kama nguo kubwa kikishuka, kikitelemushwa mpaka chini, kikishikwa kwenye pembe zake ine.


Naye Stefano akasema: “Ninaona mbingu zimefunguliwa wazi, naye Mwana wa Mutu akisimama na mamlaka karibu na Mungu.”


Siku moja ya kumwabudu Bwana, nikashikwa na Roho wa Mungu, nikasikia sauti kubwa, inayolia kama baragumu,


Basi nikageuka kusudi nione yule aliyesema nami. Na wakati nilipogeuka nikaona vinara saba vya taa vilivyotengenezwa na zahabu.


Basi uandike mambo unayoona, na mambo yanayokuwa sasa na yale yatakayotokea nyuma.


Manabii hao wawili wakasikia sauti kubwa toka mbinguni ikiwaambia: “Mupande huku!” Wakapanda mbinguni wakizungukwa na wingu, wale waadui zao wakiwa wakiwaangalia.


Kisha hekalu la Mungu linalokuwa mbinguni likafunguliwa, na Sanduku la Agano lake likaonekana ndani yake. Halafu kukatokea umeme, makelele, ngurumo ya radi, tetemeko la inchi na mvua kubwa ya mawe.


Malaika wa saba akamwanga kikombe chake katika anga. Halafu sauti kubwa ikasikilika kutoka katika hekalu kwenye kiti cha kifalme ikisema: “Sasa ni mwisho!”


Kisha nikaona mbingu imefunguka na kukatokea farasi mweupe. Yule aliyepanda juu yake anaitwa Mwaminifu na Mwenye Ukweli, kwa maana anahukumu na kupigana vita kwa haki.


Kisha yule malaika akaniambia: “Maneno haya ni ya kweli na ya uhakika. Na Bwana Mungu anayewaongoza manabii kwa njia ya Roho wake ametuma malaika wake kwa kuwaonyesha watumishi wake mambo yanayopaswa kutokea kisha kidogo.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ