Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ufunuo 3:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Angalia, nitakupa watu wa kikundi chenye kuabudu Shetani, ndio wale wasema uongo wanaojidai kwamba wao ni Wayuda, lakini ni wadanganyifu. Hakika nitawalazimisha kupiga magoti mbele yako, nao watajua ya kuwa mimi ninakupenda.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ufunuo 3:9
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Katika kila jimbo na kila muji, popote pale tangazo hili liliposomwa, Wayuda wakafurahi na kushangilia, wakafanya sherehe na mapumziko; na watu wengine wengi wakajifanya kuwa Wayuda, maana waliwaogopa sana Wayuda.


Musa akamalizia kwa kumwambia mufalme: “Watumishi wako hawa watanifikia na kuinama mbele yangu kwa heshima, wakinisihi niondoke katika inchi ya Misri, mimi pamoja na watu wote wanaonifuata. Nyuma ya hayo, nitaondoka.” Kisha Musa, akiwa amekasirika, akaondoka kwa mufalme wa Misri.


Ninyi ni wa bei kali mbele yangu, ninawaheshimu na kuwapenda. Kwa hiyo, ninatoa watu kusudi niwapate ninyi, ninayaachilia mataifa pahali pa maisha yenu.


Yawe anasema hivi: Utajiri wa Misri na faida ya uchuuzi za Kushi, pamoja na za watu wa Seba, wale watu warefu sana, zitakuja kwako mwenyewe wewe taifa la Israeli, zote zitakuwa mali yako. Watu hao watakufuata wakifungwa minyororo; watainama mbele yako na kukusihi wakisema: Kwako kuna Mungu wa kweli, wala hakuna Mungu mwingine lakini yeye.


Wafalme watakushugulikia, na malkia watakutengenezea chakula. Watainama mbele yako uso mpaka chini, na kulambula mavumbi ya miguu yako. Halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe; wote wanaonitegemea hawatapata haya.


Wazao wa wale waliokutesa, watakuja na kuinama uso mpaka chini mbele yako. Wote wale waliokuzarau, watapiga magoti kwenye miguu yako. Watakuita: “Muji wa Yawe”, “Sayuni”, “Muji wa Mutakatifu wa Israeli”.


Ninaomba nikuwe ndani yao na wewe ndani yangu, kusudi wapate kuwa mumoja kabisa; na dunia ijue kama wewe ndiwe uliyenituma na kwamba unawapenda kama vile unavyonipenda.


Ninajua mateso yako na umasikini wako, lakini wewe ni tajiri! Vilevile ninajua jinsi unavyotukanwa na wale wanaojidai kuwa Wayuda lakini si Wayuda; wao ni kikundi cha wenye kuabudu Shetani!


Yeyote atakayebakia katika jamaa yako atamwendea kuhani yule na kumwomba kikoroti cha feza au mukate, na kumwambia: Ninakuomba uniweke kwenye nafasi moja ya kuhani kusudi niweze kupata tu kipande cha mukate.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ