Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ufunuo 3:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Basi ukumbuke mafundisho uliyopokea na yale uliyosikia. Uyashike na kugeuka toka zambi zako. Kama usipokesha, nitakuja kama mwizi, wala hautajua saa nitakapokuja kwako.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ufunuo 3:3
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Huko ndiko mutakapokumbuka mwenendo wenu na matendo yenu mabaya ambayo yaliwachafua; nanyi mutachukizwa kabisa kwa sababu ya maovu yote muliyotenda.


Kisha mutakapokumbuka mienendo yenu miovu na matendo yenu mabaya, mutajichukia wenyewe kwa sababu ya maovu yenu na machukizo muliyofanya.


Na Yesu akaongeza kusema: “Basi mukeshe, kwa sababu hamujui siku wala saa ile.


Mujiangalie, mukeshe, kwa maana hamujui saa wakati ule utakapotimia.


Mujiangalie, asikuje kwa rafla na kuwakuta mumelala usingizi.


Kwa maana munajua ninyi wenyewe kwamba siku Bwana atakaporudia, itatimia kwa saa musiyozania kama vile mwizi anavyokuja usiku.


Timoteo, uchunge vizuri kile ulichopewa kwa kulinda, ukiepuka maneno ya kidunia na mabishano yasiyokuwa na maana juu ya ile watu wengine wanayoita kuwa ni elimu lakini ni uongo.


Ushike maneno ya kweli niliyokufundisha, yapate kuwa mufano kwako. Ushikamane na imani na upendo unaokuwa nao kwa njia ya kuungana kwako na Kristo Yesu.


Kwa sababu hiyo, tunapaswa kushikamana zaidi na habari tuliyosikia, kusudi tusipotee mbali.


Ninaona kwamba ni vema niwaamushe kwa njia ya kuwakumbusha mambo haya wakati wote wa maisha yangu.


Wapendwa wangu, hii ni sasa barua ya pili ninawaandikia. Katika barua hizi zote mbili nilitaka kuamusha ndani yenu mafikiri safi mupate kukumbuka mambo haya.


Siku Bwana atakaporudi, itatimia kama vile mwizi anavyokuja. Siku ile mbingu zitatoweka kwa shindo kubwa, na viumbe vyote vinavyoangaza katika mbingu vitayeyuka. Dunia na vitu vyote vinavyokuwa ndani yake vitateketezwa.


“Sikiliza, ninakuja kwa saa isiyozaniwa kama vile mwizi. Heri yule anayekesha na kutunza nguo zake vizuri kusudi asitembee uchi na kujifezehesha mbele ya watu.”


Lakini ninawaomba tu mushikamane na kile munachokuwa nacho mpaka nitakapokuja.


Basi kumbuka jinsi ulivyokuwa ulipokuwa haujaanguka, ugeuke toka zambi zako na kurudilia yale matendo yako ya kwanza. Kama usipogeuka toka zambi zako, nitakuja kwako na kuongoa kinara chako toka pahali pake.


Yesu anasema: “Sikiliza, ninakuja upesi! Heri yule anayeshika maneno ya unabii yanayoandikwa katika kitabu hiki!”


Ninakuja upesi. Shika sana kile unachokuwa nacho, kusudi mutu yeyote asinyanganye taji yako ya ushindi.


Mimi ninawaonya na kuwaazibu wote ninaowapenda. Basi ufanye nguvu, ugeuke toka katika zambi.


Amuka! Uimarishe kile kinachobaki kinachokaribia kufa, kwa maana nimeona kwamba matendo yako si makamilifu mbele ya Mungu wangu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ