Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ufunuo 3:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Amuka! Uimarishe kile kinachobaki kinachokaribia kufa, kwa maana nimeona kwamba matendo yako si makamilifu mbele ya Mungu wangu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ufunuo 3:2
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Maana, alipokuwa muzee, wake zake walimupotosha hata akaitumikia miungu mingine, wala hakukuwa mwaminifu kabisa kwa Yawe, Mungu wake, kama baba yake Daudi alivyokuwa mwaminifu.


Abiyamu alitenda zambi zilezile baba yake alizotenda, wala hakukuwa na moyo mwaminifu kwa Yawe, Mungu wake, kama babu yake Daudi alivyokuwa.


Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe ingawa hakutenda kwa moyo mukamilifu.


Ningeweza kuwatia moyo kwa maneno yangu, na maneno yangu ya faraja yangewatuliza.


Muimarishe mikono zaifu, mukaze magoti yanayoregea.


Maana walinzi wa Israeli wote ni vipofu; wote hawana akili yoyote. Wote ni kama imbwa bubu wasioweza kufoka, wanalala tu na kuota ndoto, wanapenda sana kusinzia!


Munafikiri kwamba munafanya sawa, lakini nitayafichua matendo yenu, nayo miungu yenu haitawafalia kitu.


Nitawatafuta kondoo waliopotea na waliotangatanga nitawarudisha kwa nyumba. Waliovunjika nitawatunza, na wale wanaokuwa zaifu nitawapatia nguvu. Lakini kondoo wanono na wenye nguvu nitawaangamiza. Mimi nitawachunga kondoo kama inavyostahili.


TEKELI: wewe umepimwa kwenye mizani, nawe ukaonekana hauna uzito wowote.


Maana nitaleta katika inchi muchungaji asiyemujali kondoo anayeangamia, au kumutafuta kondoo anayetangatanga, au kumutunza aliyeumizwa wala kumukulisha yule anayekuwa muzima: lakini atakula wale kondoo wanono, hata kwato zao.


Wanafanya matendo yao yote tu kusudi wajionyeshe mbele ya watu. Wanajifungia kwa paji za nyuso vibweta vipana vyenye vikaratasi vya Maandiko Matakatifu. Nao wanavaa kanzu zenye pembe ndefu.


Na Yesu akaongeza kusema: “Basi mukeshe, kwa sababu hamujui siku wala saa ile.


Halafu wale wabinti kumi wakaamuka, wakatengeneza taa zao.


Alipokwisha kukaa Antiokia kwa siku chache, akaondoka kule, akapita muji kwa muji toka katika inchi ya Galatia mpaka katika inchi ya Furigia, na kule akawatia wanafunzi nguvu.


Lakini umupe Yoshua maagizo, umutie moyo na kumwimarisha, maana yeye ndiye atakayewaongoza watu hawa mpaka ngambo, kurizi inchi utakayoiona’.


Mwisho wa vitu vyote unakaribia kutimia. Kwa hiyo mukuwe wenye akili na waangalifu, kusudi mukuwe na uwezo wa kuomba.


Mukuwe waangalifu na mukeshe, kwa maana adui yenu Shetani anazungukazunguka kama simba anayenguruma akitafuta yule atakayerarua.


“Sikiliza, ninakuja kwa saa isiyozaniwa kama vile mwizi. Heri yule anayekesha na kutunza nguo zake vizuri kusudi asitembee uchi na kujifezehesha mbele ya watu.”


Lakini niko na neno moja juu yako: wewe hauna tena upendo kwangu kama vile mbele.


“Umwandikie malaika wa kanisa la Sardi hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayekuwa na roho zile saba za Mungu na zile nyota saba. Ninajua matendo yako, hakika wewe umekwisha kufa ingawa unajulikana kuwa muzima.


Basi ukumbuke mafundisho uliyopokea na yale uliyosikia. Uyashike na kugeuka toka zambi zako. Kama usipokesha, nitakuja kama mwizi, wala hautajua saa nitakapokuja kwako.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ