Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ufunuo 2:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 “Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda nitamupa ruhusa ya kula matunda ya muti wa uzima unaokuwa katika bustani ya Mungu!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ufunuo 2:7
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe Mungu akaotesha kutoka udongo kila aina ya miti ya kupendeza macho na inayofaa kwa chakula. Katikati ya bustani hiyo kulikuwa muti wa uzima na muti wa kujua mazuri na mabaya.


Tunda la mwenye haki ni muti wa uzima, na mwenye hekima anavuta watu.


Tumaini la kungojangoja linaumiza moyo, lakini tazamio linalotimia ni musingi wa uzima.


Ulimi mupole ni musingi wa uzima, lakini uovu wake unavunja moyo.


Hekima ni muti wa uzima kwa wote wanaoipata; wana heri wote wanaoshikamana nayo.


Ulikaa Edeni, bustani ya Mungu. Ulipambwa kwa kila namna ya mawe ya bei kali, akiki, topazi, yaspi, zabarajadi, berili, sardoniki, yakuti samawi, almasi na zumaridi. Ulikuwa na mapambo ya zahabu. Yote uliwekewa tayari siku ulipoumbwa.


Kati ya miti ya mierezi ya bustani ya Mungu, hakuna muti uliolingana nao, wala misunobari haikulingana na matawi yake, mibambakofi haikuwa na matawi kama yake, hata muti wowote wa bustani ya Mungu haukulingana nao kwa uzuri.


Mwenye kuwa na masikio ya kusikia, asikie!


Lakini wenye haki watametameta kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Mwenye kuwa na masikio ya kusikia, asikie!”


Basi mwenye kuwa na masikio ya kusikia, asikie!”


Kisha akawaambia: “Mwenye kuwa na masikio ya kusikia, asikie!”


Hakuna kitu kinachoingia ndani ya mutu kutoka inje kinachoweza kumuchafua. Lakini kitu kinachotoka ndani yake ndicho kinachomuchafua. [


Mwenye kuwa na masikio ya kusikia, asikie.]”


Yesu akamujibu: “Kweli ninakuambia wewe: leo hii utakuwa pamoja nami katika Paradizo.”


Lakini mbegu zingine zikaanguka katika udongo muzuri; nazo zikaota na kutoa matunda, kila moja punje mia.” Yesu alipokwisha kuwaambia hayo yote, akasema: “Mwenye kuwa na masikio ya kusikia, asikie!”


Nimewaambia maneno haya kusudi mukuwe na amani, mukibaki katika umoja nami. Mutapata mateso katika dunia. Lakini mujipe moyo, kwa kuwa mimi nimepata ushindi juu ya vyote katika dunia.”


Lakini Mungu ametufunulia sisi siri yake kwa njia ya Roho wake. Maana Roho anachunguza vitu vyote, hata mipango ya Mungu inayofichwa kabisa.


Katika Paradizo, mutu yule akasikia mambo ya ajabu na yasiyoruhusiwa kwa mwanadamu kuyaeleza.


Ninawaandikia ninyi wababa, kwa sababu mumemujua yule aliyekuwa tangu mwanzo wa vitu vyote. Ninawaandikia ninyi vijana kwa sababu mumemushinda yule Mwovu.


Tena nikasikia sauti kutoka mbinguni, ikisema: “Andika maneno haya: ‘Heri tangu sasa kwa watu wanaokufa wakimwamini Bwana!’ ” Naye Roho anasema: “Ndiyo, ni kweli. Watapumzika toka katika masumbuko yao, kwa maana matendo yao yatafuatana nao.”


Tena nikaona kitu kinachofanana na bahari ya kioo, iliyochanganyika na moto. Nikaona vilevile wale walioshinda yule nyama wa ajabu pamoja na sanamu yake na tarakimu zinazolingana na herufi za jina lake. Watu wale walikuwa wakisimama juu ya ile bahari ya kioo wakishika vinubi walivyopewa na Mungu.


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoambia makanisa! “Yule atakayeshinda hatapatwa na kifo cha pili.


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda, nitamupa ile mana iliyofichwa. Na nitamupa vilevile jiwe dogo jeupe, na juu yake kumeandikwa jina jipya ambalo hakuna mutu yeyote anayelijua, isipokuwa tu yule anayelipewa.


Yule atakayeshinda atapokea toka kwangu zawadi ile, mimi nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwana wangu.


Heri wale wanaosafisha kanzu zao, kwa maana watakuwa na haki ya kukula matunda ya muti wa uzima na ya kuingia katika muji ule kwa kupitia kwenye milango.


Roho na Bibi arusi wanasema: “Kuja!” Naye mwenye kusikia maneno haya aseme vilevile: “Kuja!” Yule anayesikia kiu akuje, na yule anayetaka maji ya uzima akuje kuyapokea kwa bure.


Muto ule ulitelemuka katikati ya barabara ya muji mutakatifu. Kandokando ya ule muto, kulikuwa kumeota muti wa uzima, nao unatoa matunda mara kumi na mbili kwa mwaka, maana yake mara moja kila mwezi. Majani ya muti ule yanatumiwa kama dawa ya kuponyesha mataifa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ