Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ufunuo 2:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Basi kumbuka jinsi ulivyokuwa ulipokuwa haujaanguka, ugeuke toka zambi zako na kurudilia yale matendo yako ya kwanza. Kama usipogeuka toka zambi zako, nitakuja kwako na kuongoa kinara chako toka pahali pake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ufunuo 2:5
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitakupatia waamuzi wanaokuwa sawa wale wa kwanza na washauri wanaokuwa sawa wale wa zamani. Halafu, Yerusalema utaitwa Muji wa Haki, Muji Mwaminifu.


Jinsi gani ulivyoporomoshwa toka mbinguni, wewe uliyekuwa nyota yenye kuangaza kwa mapambazuko. Jinsi gani ulivyoangushwa chini, wewe uliyeyashinda mataifa!


Huko ndiko mutakapokumbuka mwenendo wenu na matendo yenu mabaya ambayo yaliwachafua; nanyi mutachukizwa kabisa kwa sababu ya maovu yote muliyotenda.


Kisha mutakapokumbuka mienendo yenu miovu na matendo yenu mabaya, mutajichukia wenyewe kwa sababu ya maovu yenu na machukizo muliyofanya.


Watu wa Samaria wataazibiwa kwa ajili ya kosa lao; wamemwasi Mungu wao. Watauawa kwa upanga, watoto wao watapondwapondwa, na wamama wenye mimba watapasuliwa tumbo.


Yawe anasema: Nilipowakuta Waisraeli walikuwa kama zabibu katika jangwa. Nilipowaona babu zenu, walikuwa bora kama matunda ya tini za kwanza. Lakini walipofika kule Bali-Peori, wakajitolea kwa kuabudu chukizo Bali, wakakuwa chukizo kama kile walichokipenda.


Hivyo, sadaka za watu wa Yuda na wa Yerusalema zitamupendeza Yawe kama za watu wa zamani; kama katika miaka iliyopita.


“Ninyi ni kama mwangaza katika dunia. Muji unaojengwa juu ya mulima hauwezi kufichama.


Hakuna mutu anayewakisha taa na kuiweka chini ya kitunga, lakini anaiweka juu ya kinara kusudi iwaangazie wote wanaokuwa ndani ya nyumba.


Kisha Yesu akauliza: “Basi yule mwenye shamba la mizabibu atafanya nini? Yeye atakuja na kuwaua wale walimaji. Na kisha atawapatia walimaji wengine shamba lile.


Atatangulia mbele ya kufika kwa Bwana, akiwa na roho na uwezo kama nabii Elia, kwa kuwapatanisha tena baba na watoto wao, na kuwageuza waasi wapate kuwa na hekima kama vile wenye haki. Hivi atamutayarishia Bwana watu wanaokuwa tayari kwa kumupokea.”


Atakuja na kuwaua wale walimaji. Na kisha atawapatia walimaji wengine shamba lile.” Watu waliposikia maneno hayo, wakasema: “Isitufikie vile hata kidogo.”


Kama munatafuta kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya kushika Sheria, mumejitenga mbali na Kristo na kujipotezea neema ya Mungu.


kusudi mupate kuwa bila kosa na kuwa na maisha safi. Hivi mutakuwa watoto wakamilifu wa Mungu wasiokuwa na kilema kati ya watu waovu na wapotovu wa dunia hii. Munapaswa kuangaza kati ya watu hawa kama vile nyota zinavyoangaza katika mbingu,


Mukumbuke mambo yaliyowatokea katika siku zilizopita. Ninyi mulipokwisha kuangaziwa na Mungu, mulipita katika mateso mengi lakini mulivumilia.


Basi ninyi wapendwa wangu, mumekwisha kutambua mambo haya. Mujiangalie vizuri kusudi musipotoshwe na makosa ya watu waovu na kukosa kusimama imara.


Basi yeye anayeweza kuwalinda kusudi musianguke, na kuwasimamisha ninyi mbele ya utukufu wake pasipo kilema na kwa furaha kubwa,


Hii ndiyo maana ya lile fumbo juu ya zile nyota saba ulizoona katika mukono wangu wa kuume, na vile vinara saba vya zahabu: zile nyota saba ni wamalaika wa makanisa saba na vile vinara saba ni yale makanisa saba.


Watu wakaunguzwa na lile joto kali, hata wakatukana jina la Mungu anayekuwa na uwezo wa kuamuru mapigo yale. Wakakataa kugeuka toka zambi zao na kumutukuza Mungu.


Basi ugeuke toka zambi zako, kwa maana kama si vile nitakuja kwako upesi, nami nitapigana na watu wale kwa upanga unaotoka ndani ya kinywa changu.


Ninajua matendo yako, upendo wako, imani yako, kazi yako na uvumilivu wako. Ninajua kwamba sasa unajitolea kwa kunitumikia kuliko mbele.


Ninajua matendo yako na taabu yako na uvumilivu wako. Ninajua kwamba hauwezi kuwakubali watu waovu. Umewapima wale wanaojiita mitume, kumbe si mitume, nawe ukatambua kwamba ni wasema uongo.


Mimi ninawaonya na kuwaazibu wote ninaowapenda. Basi ufanye nguvu, ugeuke toka katika zambi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ