Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ufunuo 18:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Ni kwa sababu mataifa yote yalileweshwa na divai kali ya uasherati wa muji ule. Wafalme wa dunia wamezini nao, na wachuuzi wa dunia wamejitajirisha kutokana na uwingi wa mali zake.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ufunuo 18:3
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ndivyo watakavyokuwa hao uliowategemea hivyo, hao uliojishugulisha nao tangu ujana wako. Watatangatanga kila mumoja njia yake; hakuna hata mumoja atakayeweza kukuokoa.


Mufalme Nebukadneza wa Babeli aliuharibu na kuuponda Yerusalema aliuacha kama chungu kitupu; aliumeza kama vile nyoka mukubwa. Alijaza tumbo lake vitu vyake vizurivizuri, akautupilia mbali kama matapiko.


Babeli ilikuwa kikombe cha zahabu katika mukono wa Yawe, ambacho kiliilewesha dunia nzima. Mataifa yalikunywa divai yake; kwa hiyo, yakapata wazimu.


Wale waliokula vyakula vinono wanakufa na njaa katika barabara. Waliolelewa na kuvalishwa namna ya kifalme wanafukua kwa mikono kwenye yalala.


Ninawe! Wewe umekuwa kama kahaba. Umewashawishi watu, ewe binti wa uchawi, uliyeyafanya mataifa kuwa watumwa kwa ukahaba wako, na watu wa mataifa kwa uchawi wako.


Basi mulienda kuangalia nini? Mutu aliyevaa nguo nzuri? Hapana! Wale wanaovaa nguo za bei kali na kuishi katika raha wanakaa katika nyumba za kifalme.


Lakini ukatae kuandika wajane wanaokuwa wangali vijana katika hesabu ile kwa maana wanapovutwa na tamaa ya kutaka kuolewa, wanaacha kumutumikia Kristo.


Malaika wa pili akafuata yule wa kwanza akisema: “Umebomoka, umebomoka kabisa, ule muji mukubwa Babeli. Umewakunywesha mataifa yote divai yake kali, ukiwalewesha na maovu ya uasherati wake.”


Wafalme wa dunia wamefanya uzinzi pamoja naye, na wakaaji wa dunia wamelewa divai ya uasherati wake.”


Wakajitupia mavumbi juu ya vichwa vyao, wakalia na kufanya kilio, nao walilalamika, wakisema: “Ole! Ole kwa muji ule mukubwa! Wote wanaokuwa na mashua za kufanya uchuuzi juu ya bahari walijitajirisha na mali zake nyingi. Lakini kwa muda wa saa moja tu umebaki mutupu.”


Mwangaza wa taa hautaonekana tena ndani yako. Na hakutasikilika tena kelele la wenye kuoa au kuolewa. Itakutokea vile kwa sababu wachuuzi wako walikuwa wenye uwezo mukubwa katika dunia, nawe umewadanganya watu wote kwa njia ya vitendo vyako vya uchawi.”


Na kwa kadiri ulivyojitukuza na kuishi katika raha, kwa kadiri ile ile muuletee mateso na huzuni. Muji ule unajisemesha: ‘Mimi ninaikaa juu ya kiti cha kifalme kama vile malkia; mimi si mujane, wala sitapata huzuni hata kidogo!’


Wafalme wa dunia waliozini nao na kujifurahisha pamoja nao wataulilia na kuufanyia kilio wakati watakapoona moshi wa moto utakaouteketeza ukipanda juu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ