Ufunuo 17:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
9 “Hapa inafaa kuwa na akili na hekima. Vile vichwa saba ni milima saba, ambavyo yule mwanamuke anaikaa juu yake. Vile vichwa ni vilevile wafalme saba.
Lakini sasa, Danieli, weka kwa siri mambo hayo; funga kitabu na kutia muhuri juu yake mpaka wakati wa mwisho utakapofika. Wengi watakimbilia huko na huko, na maarifa yataongezeka.
Enyi watu wa Efuraimu, muko na maneno gani tena na sanamu? Mimi ndiye ninayesikiliza maombi yenu, mimi ndiye ninayewatunza. Mimi nitawapa kivuli kama cha muti wa muberoshi; kutoka kwangu mutapata matunda yenu.
“Mutamwona yeye anayeitwa ‘Chukizo Linaloleta Uharibifu,’ yule aliyetajwa na nabii Danieli, akisimamishwa katika hekalu. (Anayesoma maneno haya aelewe maana yake.)
Kisha nikaona nyama mumoja wa ajabu akitokea ndani ya bahari. Alikuwa na vichwa saba na pembe kumi. Na juu ya kila pembe lake kulikuwa taji, na juu ya vichwa vile kulikuwa kumeandikwa jina la kumutukana Mungu.
Hapa inafaa kuwa na hekima. Yule anayekuwa na akili afafanue hesabu ya tarakimu zinazolingana na jina la yule nyama, kwa maana tarakimu ile ni ya mutu fulani. Nayo ni mia sita makumi sita na sita.
Nikashikwa na Roho wa Mungu, na malaika akanipeleka katika jangwa. Kule nikaona mwanamuke aliyekuwa akiikaa juu ya nyama mumoja wa ajabu mwekundu aliyeandikwa juu yake majina ya kumutukana Mungu. Nyama yule alikuwa na vichwa saba na pembe kumi.
Halafu yule malaika akaniuliza: “Kwa nini unashangaa? Nitakuambia maana ya fumbo la mwanamuke yule na ya yule nyama anayemubeba, na anayekuwa na vichwa saba na pembe kumi.