Ufunuo 16:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
3 Malaika wa pili akamwanga kikombe chake katika bahari. Maji yakageuka na kuwa kama damu ya mufu, na viumbe vyote vyenye uzima vilivyokuwa ndani ya bahari vikakufa.
Nao wako na uwezo wa kufunga mbingu kusudi mvua isinyeshe wakati wanapotangaza ujumbe wa Mungu. Wako vilevile na uwezo wa kugeuza maji kuwa damu, na uwezo wa kuleta mapigo ya kila namna kila wakati wanapotaka.
Kisha nikaona nyama mumoja wa ajabu akitokea ndani ya bahari. Alikuwa na vichwa saba na pembe kumi. Na juu ya kila pembe lake kulikuwa taji, na juu ya vichwa vile kulikuwa kumeandikwa jina la kumutukana Mungu.