Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ufunuo 15:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Waliimba wimbo wa Musa, mutumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana- Kondoo wakisema: “Ewe Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo, matendo yako ni makubwa na ya ajabu! Ewe Mufalme wa mataifa, kazi zako ni za haki na za kweli!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ufunuo 15:3
49 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati Abramu alipokuwa na umri wa miaka makumi tisa na tisa, Yawe akamutokea, akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Uwezo. Uendelee mbele yangu na kuwa mukamilifu.


Kwa njia hii watu wa Israeli waliwapa Walawi miji kusudi waishi ndani yake pamoja na mashamba ya malisho ya miji hiyo.


Basi mufalme akamwita kiongozi Yoyada, akamwuliza: “Mbona haujaamurisha Walawi kukusanya kutoka kwa watu wa Yuda na Yerusalema, kodi ambayo Musa mutumishi wa Yawe aliagiza watu walipe kwa ajili ya Hema Takatifu la Yawe?”


Kwa njia ya Musa, mutumishi wako, ukawajulisha siku zako za Sabato takatifu na ukawaagiza kuzifuata amri, masharti na sheria ulizowaamuru.


Usisahau kusifu matendo yake ambayo watu wameyashangilia.


yeye anayetenda mambo makubwa yasiyochunguzika, anayetenda maajabu yasiyohesabika.


Yawe ni muzuri! Wema wake unadumu milele, na uaminifu wake kwa vizazi vyote.


Mukumbuke matendo ya ajabu aliyotenda, miujiza yake na hukumu alizotoa,


Matendo ya Yawe ni makubwa sana! Wote wanaoyafurahia wanayachunguza.


Matendo yake ni ya haki na ya kuaminika; kanuni zake zote ni za kutegemewa siku zote.


Ninakusifu maana umeniumba kwa namna ya ajabu. Matendo yako ni ya ajabu. Wewe unanijua kabisa kabisa.


Yawe ni mwenye haki katika njia zake zote; ni mwema katika matendo yake yote.


Watu watatangaza ukubwa wa matendo yako ya ajabu, nami nitatangaza ukubwa wako.


Kwa musaada wako, ninashinda kundi la waaskari; kwa musaada wa Mungu wangu, ninaruka kuta.


Alifanya maajabu mbele ya babu zao, katika mbuga za Soani kule Misri.


Ee Yawe, matendo yako makubwa yananifurahisha; nitashangilia kwa sababu ya mambo yote uliyotenda.


Ee mufalme mukubwa, mupenda haki, umesimamisha usawa katika Israeli; umeleta sheria na haki.


Maana Yawe ni mwamuzi wetu, yeye ni mutawala wetu; Yawe ni mufalme wetu, yeye ndiye anayetuokoa.


Mutangaze na kusema habari zenu. Mufanye shauri pamoja! Ni nani aliyetangaza zamani matukio ya sasa? Ni nani aliyesema mambo haya zamani? Haikukuwa mimi Yawe? Hakuna Mungu mwingine isipokuwa mimi! Mimi ni Mungu wa haki na mwokozi; hakuna mwingine isipokuwa mimi.


Ilipokuwa asubui mapema, mufalme Dario aliamuka, akaenda kwa haraka kwenye pango la simba.


Waisraeli wote wameiasi sheria yako, wamekuacha wakakataa kukutii. Kwa sababu tumekukosea, tumemwangiwa laana na viapo vilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, mutumishi wako.


Enyi watu wa Efuraimu, muko na maneno gani tena na sanamu? Mimi ndiye ninayesikiliza maombi yenu, mimi ndiye ninayewatunza. Mimi nitawapa kivuli kama cha muti wa muberoshi; kutoka kwangu mutapata matunda yenu.


Utatuonyesha uaminifu na wema wako sisi wazao wa Abrahamu na wa Yakobo, kama ulivyowaahidi babu zetu tangu zamani.


Lakini Yawe anayekuwa katika muji ule ni mwenye haki, yeye hatendi jambo lolote baya. Kila siku asubui anatangaza hukumu yake, kila kunapopambazuka anaitimiza. Lakini waovu hawana haya hata kidogo.


Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.


Sheria ya Mungu ilitolewa kwa njia ya Musa, lakini neema na ukweli vilikuja kwa njia ya Yesu Kristo.


Halafu, Musa akasema maneno ya wimbo huu mbele ya kusanyiko lote la Waisraeli.


Maana nitatangaza jina la Yawe, nanyi museme: “Mungu wetu ni Mukubwa”.


Basi, Musa mutumishi wa Yawe akakufa kule katika inchi ya Moabu kulingana na neno Yawe alilosema.


Kwa Mufalme wa milele, asiyeweza kufa, asiyeonekana, Mungu peke yake, ikuwe heshima na utukufu milele na milele! Amina.


Musa alikuwa mutumishi mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu, kusudi ashuhudie maneno ambayo Mungu angesema nyuma.


Mukuwe waangalifu kutii amri na sheria ambazo Musa, mutumishi wa Yawe, aliwaamuru: mumupende Yawe, Mungu wenu, mufuate anachotaka na kushika amri zake, mukae pamoja naye na kumutumikia kwa moyo wote na roho yote.”


Bwana Mungu Mwenye Uwezo anasema: “Mimi ni Alfa na Omega.” Ni yeye anayekuwa, aliyekuwa na anayekuja.


wakisema: “Tunakushukuru wewe Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo, unayekuwa na uliyekuwa, kwa maana umetumia uwezo wako mukubwa nawe ukasimika ufalme wako.


Wale watu elfu mia moja makumi ine na ine waliimba wimbo mupya mbele ya kile kiti cha kifalme na mbele ya vile viumbe vine vya ajabu na ya wale wazee. Hakuna mutu aliyeweza kujifunza wimbo ule, isipokuwa wale watu elfu mia moja makumi ine na ine waliokombolewa katika dunia.


Malaika wa pili akafuata yule wa kwanza akisema: “Umebomoka, umebomoka kabisa, ule muji mukubwa Babeli. Umewakunywesha mataifa yote divai yake kali, ukiwalewesha na maovu ya uasherati wake.”


Watapigana vita na Mwana-Kondoo, lakini Mwana-Kondoo pamoja na waaminifu wake aliowaita na kujichagulia atawashinda, kwa sababu yeye ni Bwana wa wabwana na Mufalme wa wafalme.”


Na juu ya nguo yake na paja la muguu wake kulikuwa kumeandikwa jina hili: “Mufalme wa wafalme na Bwana wa wabwana.”


Hukumu zake ni za kweli na za haki. Amehukumu yule kahaba mukubwa ambaye alikuwa akipotosha dunia kwa vitendo vyake vya uasherati. Mungu amemulipiza kisasi cha damu ya watumishi wake!”


Na kila kimoja cha viumbe vya ajabu kilikuwa na mabawa sita yenye kujaa macho ndani na inje. Navyo viliimba muchana na usiku bila kuchoka, vikisema: “Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo, aliyekuwa, anayekuwa na anayekuja.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ