Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ufunuo 14:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Wale watu elfu mia moja makumi ine na ine waliimba wimbo mupya mbele ya kile kiti cha kifalme na mbele ya vile viumbe vine vya ajabu na ya wale wazee. Hakuna mutu aliyeweza kujifunza wimbo ule, isipokuwa wale watu elfu mia moja makumi ine na ine waliokombolewa katika dunia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ufunuo 14:3
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mupya; nitakupigia kinubi cha nyuzi kumi,


Haleluia! Mumwimbie Yawe wimbo mupya; mumusifu katika kusanyiko la waaminifu!


Yawe ni rafiki ya wale wanaomwabudu; yeye anawajulisha agano lake.


Mumwimbie wimbo mupya; mupige kinubi vizuri na kushangilia.


Aliniondoa katika shimo la hatari, alinitoa katika matope mengi, akanisimamisha salama juu ya mulima, na kuziimarisha hatua zangu.


Mumwimbie Yawe wimbo mupya! Mumwimbie Yawe, ninyi ulimwengu wote!


Zaburi. Mumwimbie Yawe wimbo mupya, kwa maana ametenda mambo ya ajabu! Nguvu yake kubwa, mukono wake mutakatifu umemupatia ushindi.


Mumwimbie Yawe wimbo mupya! Dunia yote iimbe sifa zake: bahari na vyote vinavyokuwa ndani yake, inchi za mbali na wakaaji wake;


Hivi, mahubiri ya kufa kwa Kristo juu ya musalaba yanahesabiwa kuwa upumbafu kwa wale wanaopotea. Lakini kwa sisi tunaookolewa ni uwezo wa Mungu.


Lakini mutu anayefuata hali yake ya kidunia hawezi kukubali maneno yanayotoka kwa Roho yule. Kwa sababu anayaona kuwa ni upumbafu kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa maana yanatambulikana tu kwa njia ya Roho.


Kisha nikaangalia, nikaona Mwana-Kondoo akisimama juu ya mulima Sayuni. Naye alikuwa pamoja na watu elfu mia moja makumi ine na ine, na juu ya paji za nyuso za watu wale kulikuwa kumeandikwa jina lake na jina la Baba yake.


Waliimba wimbo wa Musa, mutumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana- Kondoo wakisema: “Ewe Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo, matendo yako ni makubwa na ya ajabu! Ewe Mufalme wa mataifa, kazi zako ni za haki na za kweli!


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda, nitamupa ile mana iliyofichwa. Na nitamupa vilevile jiwe dogo jeupe, na juu yake kumeandikwa jina jipya ambalo hakuna mutu yeyote anayelijua, isipokuwa tu yule anayelipewa.


Nao walikuwa wakiimba wimbo huu mupya wakisema: “Wewe unastahili kukamata kizingo cha karatasi, na kuvunja vifundo vya mihuri yake. Kwa sababu wewe uliuawa, na kwa njia ya damu yako, ulikomboa kwa ajili ya Mungu watu wa kila kabila, wa kila luga, wa kila jamaa na wa kila taifa.


Nikasikia hesabu ya watu waliopigwa chapa ya muhuri wa Mungu ilikuwa: elfu mia moja na makumi ine na ine kutoka makabila yote ya Waisraeli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ