Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ufunuo 13:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Kimoja cha vichwa vya yule nyama kilionekana kwamba kilikuwa kimeumizwa vibaya sana, lakini kidonda kilichokuwa cha hatari ya kufa kilikuwa kimekwisha kupona. Na kwa hiyo watu wote wa dunia wakashangaa na kumufuata yule nyama.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ufunuo 13:3
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitaitia mikono ya mufalme wa Babeli nguvu na kutia upanga wangu katika mukono wake. Lakini nitaivunja mikono ya Mufalme wa Misri, naye atalalamika mbele ya mufalme wa Babeli kama mutu aliyeumizwa vibaya sana.


Katika siku zile, Augusto, mufalme wa Roma akatoa amri kwamba wafanye hesabu ya watu wa utawala wake wote.


Basi Wafarisayo wakasemezana hivi: “Hamwoni kwamba hatuwezi kufanya kitu? Angalia, dunia nzima inamufuata!”


Hata Simoni vilevile akaamini na kubatizwa. Na nyuma ya pale alishikamana na Filipo, naye alishangaa sana alipoona kitambulisho kikubwa na miujiza iliyokuwa ikifanyika.


Yeye alitumikisha mamlaka yote aliyopewa na yule nyama wa kwanza mbele yake. Alilazimisha vyote vinavyokuwa katika dunia pamoja na wakaaji wake kumwabudu yule nyama wa kwanza aliyekuwa na kovu la kidonda cha hatari.


Akawadanganya wakaaji wa dunia kwa njia ya vitambulisho alivyowezeshwa kuonyesha mbele ya yule nyama mukubwa wa kwanza. Aliwaambia watu wa dunia watengeneze sanamu kwa heshima ya yule nyama aliyeumizwa kwa upanga, lakini aliendelea kuishi.


Watano kati yao wamekwisha kuangushwa chini, mumoja angali anatawala na mwingine hajafika bado; naye atakapofika, atabaki kwa muda mufupi tu.


Yule nyama aliyekuwa yuko zamani, lakini sasa hayuko tena, yeye mwenyewe ni mufalme wa nane, ni mumoja wa wale saba naye anakwenda kuangamia kabisa.


Hawa wote kumi wako na shabaha moja ya kumupa yule nyama uwezo wao na mamlaka yao.


Kwa maana Mungu ametia ndani yao nia ya kuwasukuma kutimiza shabaha yake nao wapate kufikia shauri moja na kumupa yule nyama madaraka yao ya kifalme mpaka maneno ya Mungu yatimie.


Nikaona kwamba yule mwanamuke amelewa kwa damu ya watu wa Mungu na ya watu waliouawa kwa sababu ya ushuhuda wao kwa ajili ya Yesu. Wakati nilipomwona nikashangaa sana.


Yule nyama uliyemwona alikuwa yuko zamani, lakini sasa hayuko tena. Naye ni tayari kupanda toka katika shimo la kuzimu na kwenda kuangamizwa kabisa. Nao wakaaji wa dunia ambao majina yao hayakupata kuandikwa katika kitabu cha uzima tangia kuumbwa kwa dunia, watashangaa wakati watakapomwona yule nyama, kwa sababu alikuwa yuko zamani lakini hayuko sasa, naye atatokea tena!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ