Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ufunuo 11:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Nao watu wa kila jamaa, wa kila kabila, wa kila luga na wa kila taifa wataangalia maiti hizo kwa muda wa siku tatu na nusu, wala hawatakubali zizikwe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ufunuo 11:9
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa pahali pake, umerudi hapa, ukakula chakula na kunywa maji pahali hapa ambapo uliambiwa usikule chakula wala kunywa maji. Basi, mwili wako hautazikwa kwenye kaburi la babu zako.’ ”


Mutu akiweza kuzaa watoto mia moja, na akiishi maisha marefu, lakini kama mutu huyo hafurahii maisha yake, wala hafanyiwi mazishi, basi ninasema mutoto aliyezaliwa amekufa ni afazali kuliko mutu yule.


Ole kwako! Unaangamiza ingawa hauangamizwi. Unadanganya ingawa haudanganywi. Utakapokwisha kuangamiza, wewe utaangamizwa! Utakapomaliza kudanganya, wewe utadanganywa.


Maiti za watu hao zitakuwa chakula cha ndege na nyama wa pori, na hapatakuwa mutu atakayewafukuza.


Kwa maana mutahukumiwa kufuatana na namna munavyowahukumu wengine, na kipimo kile munachowapimia wengine ndicho kitakachotumiwa kwenu vilevile.


Kisha wakaniambia: “Imekupasa kutoa unabii tena kwa jamaa, kwa mataifa, kwa watu wa kila luga na kwa wafalme wengi.”


Lakini nyuma ya zile siku tatu na nusu, pumzi ya uzima inayotoka kwa Mungu ikaingia ndani ya maiti zao, nao wakasimama. Na watu wote waliowaona wakashikwa na woga mukubwa.


Akapewa ruhusa ya kupigana vita na watu wa Mungu na kuwashinda. Akapewa hata mamlaka ya kutawala watu wote, wa kila kabila, kila jamaa, kila luga na kila taifa.


Yule malaika akaniambia tena: “Yale maji uliyoona pale yule kahaba anapoikaa, ni watu wa kila taifa, kila jamaa na kila luga.


Wakati alipokuwa amekwisha kukamata kizingo, vile viumbe vine vya ajabu na wale wazee makumi mbili na wane wakainama uso mpaka chini mbele ya Mwana-Kondoo. Kila mumoja wao alikuwa na kinubi na vikombe vya zahabu vilivyojaa marasi, ndiyo maombi ya watu wa Mungu.


Nao walikuwa wakiimba wimbo huu mupya wakisema: “Wewe unastahili kukamata kizingo cha karatasi, na kuvunja vifundo vya mihuri yake. Kwa sababu wewe uliuawa, na kwa njia ya damu yako, ulikomboa kwa ajili ya Mungu watu wa kila kabila, wa kila luga, wa kila jamaa na wa kila taifa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ