Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ufunuo 11:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Lakini uache kiwanja kinachokuwa inje ya hekalu, usikipime kwa maana kimetolewa kwa watu wa mataifa mengine watakaokanyaga muji mutakatifu kwa muda wa miezi makumi ine na miwili.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ufunuo 11:2
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Zaburi ya Asafu. Ee Mungu, watu wasiokujua wameshambulia inchi yako. Wamechafua hekalu lako takatifu, wameugeuza Yerusalema kuwa mabomoko.


Ninyi munaona utukufu kujiita watu wa muji mutakatifu, na kujidai kumutegemea Mungu wa Israeli, ambaye jina lake ni Yawe wa majeshi.


Na sasa nitawaambia jinsi nitakavyolifanya hilo shamba langu. Nitaubomoa upango wake, nalo litaharibiwa. Nitaubomoa ukuta wake, nalo litakanyagwakanyagwa.


Amuka! Amuka! Ujipatie zile nguvu zako, ewe Sayuni! Uvae nguo yako nzuri, ewe Yerusalema, muji mutakatifu. Maana hawataingia tena kwako watu wasiotahiriwa na wachafu.


Waadui wamenyoosha mikono yao, wapate kukamata vitu vyake vyote vya bei kali. Kweli umeona watu wa mataifa wakiingia ndani ya hekalu, watu ambao Yawe aliwakataza kuingia kati kusanyiko lake.


Utakapotimiza siku hizo, utalalia kwa upande wa kuume, na hapo utabeba azabu ya watu wa ufalme wa Yuda kwa muda wa siku makumi ine; nimekupangia siku moja kuwa sawa na mwaka mumoja.


Hivyo akakuwa amepima pande zote, nazo zilikuwa metre mia mbili makumi tano kila upande. Ukuta huo ulitenganisha kati ya eneo takatifu na lile la kawaida.


Yule mutu aliyesimama upande wa juu wa muto, aliyevaa nguo za kitani, akainua mikono yake yote miwili kuelekea mbinguni. Kisha nikamusikia akiapa kwa jina la yule anayeishi milele: Itakuwa muda wa nyakati tatu na nusu. Wakati mateso ya watu watakatifu yatakapokomeshwa, mambo haya yote yatakuwa yametimia.


Kisha nikataka nielezwe juu ya yule nyama wa ine, ambaye alikuwa tofauti kabisa na wale wengine, wa kutisha sana, mwenye meno ya chuma na makucha ya shaba, aliyekula na kuvunjavunja, na kukanyagakanyaga yaliyobaki.


Huyo atasema maneno ya kujivuna mbele ya Mungu Mukubwa na kuwatesa watakatifu wake. Atajaribu kubadilisha sikukuu na sheria zao, na watakatifu watatiwa katika mikono yake kwa muda wa miaka mitatu na nusu.


Pembe dogo ile ilikomaa sana kufikia viumbe vya mbinguni; ikaangusha chini sehemu ya nyota na kuzikanyagakanyaga.


Kisha, nikamusikia mutakatifu mumoja akizungumuza na mwenzake. Huyo mwenzake alimwuliza: Matukio ya mambo yaliyotangazwa katika maono haya yataendelea kwa muda gani? Kwa muda gani sadaka za kuteketezwa za kila siku zitaendelea kuzarauliwa? Kwa muda gani upotovu wa kuangamiza kila kitu utaendelea, na Pahali Patakatifu pamoja na viumbe vya mbingu vitaendelea kukanyagwa?


Yule mutakatifu wa kwanza akamujibu: Kwa muda wa nyakati za magaribi na asubui elfu mbili mia tatu. Kisha hekalu la Mungu litapata tena hali yake kamili.


Kutokana na makosa yenu, mutataabika kwa muda wa miaka makumi ine, sawa na zile siku makumi ine mulizopeleleza ile inchi, mwaka mumoja kwa kila siku moja; mutatambua kwamba mimi nimechukizwa.


Wakatoka ndani ya makaburi, na nyuma ya kufufuka kwa Yesu, wakaingia katika muji mutakatifu Yerusalema, na watu wengi wakawaona.


Halafu Shetani akamupeleka katika Yerusalema, muji mutakatifu, akamusimamisha kwenye pembe la juu sana la hekalu, na kumwambia:


“Ninyi ni kama chumvi kwa watu wote. Lakini kama chumvi ikipoteza onjo lake, itatiwa nini ipate tena kukolea? Haifai tena hata kidogo, inabakilia kutupwa na kukanyagwa na watu.


Wamoja watauawa kwa vita na watapelekwa kuwa wafungwa katika inchi za mataifa yote. Vilevile mataifa mengine yatautawala Yerusalema mpaka nyakati zao za kuutawala zitakapokwisha.”


Basi munazania itakuwa namna gani? Hataazibiwa vikali zaidi yule anayemuzarau Mwana wa Mungu na kuihesabu kuwa bure damu ya agano la Mungu iliyomutakasa na kumutukana Roho wa neema?


Lakini nyuma ya zile siku tatu na nusu, pumzi ya uzima inayotoka kwa Mungu ikaingia ndani ya maiti zao, nao wakasimama. Na watu wote waliowaona wakashikwa na woga mukubwa.


Nami nitawatuma washuhuda wangu wawili, wakiwa wamevaa nguo za kilio. Nao watatangaza ujumbe wa Mungu kwa muda wa siku elfu moja mia mbili na makumi sita.”


Na yule mwanamuke akakimbilia katika jangwa kwenye nafasi Mungu aliyomutayarishia kusudi apate kulishwa kule kwa muda wa siku elfu moja mia mbili makumi sita.


Nikashikwa na Roho, na malaika akanipeleka juu ya mulima mukubwa na murefu. Akanionyesha muji mutakatifu, ndio Yerusalema uliokuwa ukishuka toka mbinguni kwa Mungu,


Nikaona muji mutakatifu, ndio Yerusalema mupya, uliokuwa ukishuka toka mbinguni kwa Mungu, nao ukitengenezwa vizuri kama vile bibi arusi aliyepambwa kwa ajili ya kwenda kukutana na mume wake.


Na kama mutu akipunguza neno kati ya maneno ya unabii yanayoandikwa katika kitabu hiki, Mungu ataondoa fungu la matunda ya muti wa uzima alilotayarishiwa, pamoja na fungu alilotayarishiwa katika ule muji mutakatifu ambavyo vimeandikwa katika kitabu hiki.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ