Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ufunuo 10:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Halafu yule malaika niliyemwona akisimama juu ya bahari na inchi kavu akainua mukono wake wa kuume juu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ufunuo 10:5
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Abramu akamwambia mufalme wa Sodoma: “Ninaapa kwa Yawe, Mungu Mukubwa, aliyeumba mbingu na dunia,


Ezra akaomba akisema: Wewe peke yako ndiwe Yawe! Ulifanya mbingu na jeshi lake lote, dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake, bahari na vyote vinavyokuwa ndani yake. Unavipatia uzima, na jeshi lote la mbinguni linakuabudu wewe.


Heri mutu anayesaidiwa na Mungu wa Yakobo, mutu anayemutumainia Yawe, Mungu wake,


Maana kwa siku sita mimi Yawe niliumba mbingu na inchi, bahari na vyote vinavyokuwa ndani yake, kisha nikapumzika siku ya saba. Kwa hiyo mimi Yawe nilibariki siku ya Sabato, nikaitakasa.


Nami nitawapeleka katika inchi ile niliyoapa kumupa Abrahamu, Isaka, na Yakobo. Nitawapa inchi hiyo ikuwe yenu. Mimi ni Yawe.’ ”


Hata hivyo, niliwaapia kulekule katika jangwa kwamba sitawaingiza katika inchi niliyowapa, inchi ya maziwa na asali na inchi nzuri kuliko inchi zote.


Hata hivyo, niliapa kulekule katika jangwa kwamba ningewapeleka katika inchi za mbali na kuwafanya waishi kati ya mataifa ya kigeni,


Maana nilipowapeleka katika ile inchi niliyoapa kuwapa, kila mara walipoona kilima kirefu au miti ya majani mengi, walianza kutoa matambiko na sadaka zao na kunichokoza. Kulekule walitoa sadaka za harufu nzuri na kutoa sadaka za kinywaji.


Nanyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe, wakati nitakapowarudisha mpaka katika inchi ya Israeli, inchi niliyoapa kuwapatia wazee wenu.


Uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siku ile nilipowachagua Waisraeli niliwaapia wazao wa Yakobo. Nilijijulisha kwao katika inchi ya Misri, nikawaapia nikisema: Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Bwana wenu Yawe anasema hivi: Ninaapa hakika kwamba watu wa mataifa yanayokuwa jirani yenu watatukanwa wao wenyewe.


Ninyi wote mutagawanyana sawa. Niliapa kuwa nitawapa babu zenu inchi hii, nayo itakuwa mali yenu.


Yule mutu aliyesimama upande wa juu wa muto, aliyevaa nguo za kitani, akainua mikono yake yote miwili kuelekea mbinguni. Kisha nikamusikia akiapa kwa jina la yule anayeishi milele: Itakuwa muda wa nyakati tatu na nusu. Wakati mateso ya watu watakatifu yatakapokomeshwa, mambo haya yote yatakuwa yametimia.


“Wandugu, kwa sababu gani munafanya mambo kama haya? Sisi vilevile ni watu, tuko sawasawa nanyi, na tunawahubiri ninyi Habari Njema kwamba muache kuabudu vitu hivi vya bure na mumugeukie Mungu mwenye uzima; yeye aliyeumba mbingu na dunia, bahari na vyote vinavyokuwa ndani yao.


Kwa maana nilipokuwa nikipitapita katika muji wenu nilichunguza nafasi zenu za kuabudia, nikaona hata mazabahu mamoja ambako waliyochora maandiko haya: ‘Kwa ajili ya mungu asiyejulikana.’ Basi yule munayemwabudu pasipo kumujua ndiye mimi ninayemuhubiri kwenu sasa.


Tangu Mungu alipoumba dunia, hali zake zisizoonekana, ni kusema uwezo wake wa milele na umungu wake, vinaonekana kupitia viumbe vyake. Kwa sababu hii watu wale hawatapata namna yoyote ya kujitetea.


Ninanyoosha mukono wangu mbinguni na kuapa: Kama vile ninavyoishi milele,


Wakati Mungu alipomupa Abrahamu ahadi, alifanya vilevile kiapo. Kwa sababu hakuna mutu mwingine mukubwa kuliko yeye kusudi ataje jina lake, akaapa kwa jina lake mwenyewe.


Mimi ni mwenye uzima. Nilikuwa nimekufa, lakini sasa mimi niko muzima kwa milele na milele. Niko na mamlaka juu ya lufu na kuzimu.


Alikuwa akishika kitabu kidogo chenye kufunguliwa. Halafu akaweka muguu wake wa kuume juu ya bahari na muguu wa kushoto juu ya inchi kavu.


Halafu akasema kwa sauti kubwa: “Mumuheshimu Mungu na kumutukuza, kwa sababu saa yake ya kuwahukumu watu imetimia. Mumwabudu yule aliyeumba mbingu na dunia, bahari na chemichemi za maji.”


Malaika wa saba akamwanga kikombe chake katika anga. Halafu sauti kubwa ikasikilika kutoka katika hekalu kwenye kiti cha kifalme ikisema: “Sasa ni mwisho!”


“Bwana wetu na Mungu wetu, wewe unastahili utukufu, heshima na uwezo, kwa maana wewe ndiwe uliyeumba vitu vyote; vile vimeumbwa na kupata kuwa kutokana na mapenzi yako.”


Vile viumbe vine vya ajabu viliimba kwa kumutukuza, kumuheshimia na kumushukuru yule aliyeikaa juu ya kiti cha kifalme, yule anayeishi kwa milele na milele. Kila mara vilipofanya vile,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ