Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ufunuo 10:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Na ngurumo zile saba zilipokwisha kusikilika, nikajitayarisha kwa kuandika. Lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni, ikiniambia hivi: “Uchunge kwa siri maneno yaliyosemwa na zile ngurumo saba.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ufunuo 10:4
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, kwenu ninyi, maono haya yote ni kama ujumbe ulioandikwa katika kitabu kilichofungwa kwa muhuri. Ukimupelekea mutu yeyote anayejua kusoma, na kumwambia “Unisomee kitabu hiki”, atasema “Siwezi kukisoma kwa sababu kimefungwa kwa muhuri.”


Yawe aliniambia hivi: Twaa ubao mukubwa, uandike juu yake maneno yanayosomeka waziwazi: “Teka haraka. Nyanganya Upesi.”


Nitalinda agizo hilo na kuchunga mafundisho hayo kati ya wafuasi wangu.


Lakini sasa, Danieli, weka kwa siri mambo hayo; funga kitabu na kutia muhuri juu yake mpaka wakati wa mwisho utakapofika. Wengi watakimbilia huko na huko, na maarifa yataongezeka.


Akanijibu: Danieli, ujiendee, maana maneno haya ni siri na yamefungwa kwa kutiwa muhuri juu yake mpaka wakati wa mwisho.


Maono ya hizo nyakati za magaribi na za asubui ambayo yameelezwa ni ya kweli. Lakini uyafiche, sababu ni siri, maana yatatokea kisha siku nyingi.


ikisema: “Andika katika kitabu mambo unayoona, na ukitume kwa makanisa ya miji saba: Efeso, Smurna, Pergamo, Tuatera, Sardi, Filadelfia na Laodikia.”


Basi uandike mambo unayoona, na mambo yanayokuwa sasa na yale yatakayotokea nyuma.


Kisha nikasikia tena sauti kutoka mbinguni ikiniambia: “Kwenda utwae kile kitabu kidogo chenye kufunguliwa katika mukono wa yule malaika anayesimama juu ya bahari na juu ya inchi kavu.”


Kisha akaniambia: “Usichunge kwa siri maneno haya ya unabii wa kitabu hiki, kwa sababu wakati wa kutimia kwa mambo haya unakaribia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ