Yawe aliniambia hivi: Simba mukali ananguruma kwa kukinga nyama aliyemukamata; hata kundi la wachungaji likiitwa kwa kumufukuza, hatishiki kwa kelele zao, wala hashituki kwa sauti zao. Ni vile Yawe wa majeshi atakavyoshuka kupigana juu ya mulima Sayuni na kilima chake.
Yawe anajitokeza kama shujaa; kama vile askari katika vita anatatanua kupigana. Anapiga kelele kubwa la vita na kujionyesha mwenye nguvu juu ya waadui zake.
Waaskari wao wananguruma kama simba; wananguruma kama simba wakali ambao wamekamata nyama wao na kuwapeleka mbali ambapo hakuna anayeweza kuwanyanganya.
Basi, wewe Yeremia utatabiri maneno haya yote juu yao, na kusema hivi: Yawe atanguruma kutoka juu, atatoa sauti yake kutoka kwenye makao yake matakatifu; atanguruma kwa nguvu kwa ajili ya watu wake, atapiga kelele kama wenye kukamua zabibu, kwa ajili ya wakaaji wote wa dunia.
Amosi alisema hivi: Yawe ananguruma toka mulima Sayuni, anavumisha sauti yake toka Yerusalema, hata mashamba ya malisho ya wachungaji yanakauka, majani ya mulima Karmeli yananyauka.
Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikinguruma kama uvumi wa maporomoko ya maji mengi na kama ngurumo kubwa ya radi. Sauti ile ilisikilika kama vile sauti ya wapiga vinubi wakati wanapopiga vinubi vyao.
Kisha nikaona tena katika mbingu kitambulisho kingine kikubwa na cha kushangaza sana. Kulikuwa wamalaika saba wanaoshika mapigo saba. Mapigo haya ndiyo yaliyokuwa ya mwisho, kwa maana ni yale Mungu atakayotumia kwa kutimiza kasirani yake.
Umeme ulipiga tokea katika kiti kile, na makelele na ngurumo ya radi vilisikilika. Mbele ya kiti kile kulikuwa kukiwaka mienge saba, na hizo ndizo zile roho saba za Mungu.
Kisha yule malaika akatwaa kile chetezo, akakijaza makaa ya moto toka kwenye mazabahu na kukitupa katika dunia. Na halafu kukakuwa ngurumo ya radi, makelele, umeme na tetemeko la inchi.