Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ufunuo 1:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Mimi ni ndugu yenu Yoane. Kwa njia ya kuungana na Yesu, ninashirikiana nanyi katika mateso, katika ufalme wake na katika kuvumilia. Mimi nilikuwa nimepelekwa katika kisanga kinachoitwa Patimo, kwa sababu nilihubiri Neno la Mungu na ukweli ulioshuhudiwa na Yesu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ufunuo 1:9
35 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Na Yesu akawaambia: “Hakika mutaubeba muzigo nitakaoubeba. Lakini kuikalisha mutu kwa upande wangu wa kuume au wa kushoto si kazi yangu. Ni Mungu peke yake atakayeweka watu aliowatayarisha kwenye nafasi zile.”


Nao wakamujibu: “Tunaweza.” Yesu akaongeza kuwaambia: “Hakika mutakunywa kikombe nitakachokunywa, na kubatizwa kama vile nitakavyobatizwa.


Nimewaambia maneno haya kusudi mukuwe na amani, mukibaki katika umoja nami. Mutapata mateso katika dunia. Lakini mujipe moyo, kwa kuwa mimi nimepata ushindi juu ya vyote katika dunia.”


Katika siku zile, kulikuwa mukutano wa wandugu waamini yapata watu mia moja makumi mbili. Basi Petro akasimama katikati yao, akasema:


Kule waliwajenga wanafunzi moyo na kuwatia nguvu wabakie katika imani wakiwaambia: “Ni sherti tupite katika mateso mengi kwa kuweza kuingia katika Ufalme wa Mungu.”


Na kama sisi ni watoto, basi tutakuwa na sehemu katika urizi ule Mungu aliowaahidi watu wake, na tutashiriki pamoja na Kristo katika urizi ule; kwa maana kama tukiteswa pamoja naye tutatukuzwa pamoja naye vilevile.


Lakini tukitumainia kitu tusichokiona, tunakingojea kwa uvumilivu.


Kwa hivi, hatuwezi kukata tumaini tunalokuwa nalo kwenu, kwa maana tunajua kwamba kwa kuwa munashiriki katika taabu yetu, munashiriki vilevile katika kufarijiwa kwetu.


Ni haki kwangu kuwa na mafikiri haya kwa ajili yenu ninyi wote, kwa sababu ninawakumbuka kila mara. Kwa maana mumeshiriki pamoja nami katika neema ile Mungu aliyonipatia, ingawa sasa niko katika kifungo hata na wakati nilipokuwa huru kutetea na kuimarisha Habari Njema.


Lakini, mumefanya vizuri kwa kushirikiana pamoja nami katika taabu yangu.


Bwana aongoze mafikiri yenu katika upendo wa Mungu na katika uvumilivu tunaopewa na Kristo.


Basi, usisikie haya ya kutoa ushuhuda kwa ajili ya Bwana wetu, wala usisikie haya kwa sababu yangu mimi ninayekuwa katika kifungo kwa ajili yake. Lakini ushiriki nami katika mateso kwa ajili ya Habari Njema, kufuatana na uwezo unaopewa na Mungu.


Munapaswa kuvumilia, kusudi mutimize mapenzi ya Mungu, na kuweza hivi kupewa kile mulichoahidiwa.


Ninawaonya wazee wa kanisa wanaokuwa kati yenu. Mimi vilevile ni muzee mwenzenu, nami ni mushuhuda wa mateso ya Kristo na zaidi ya hii nitashiriki katika utukufu ule utakaotokea.


Hizi ni habari za mambo yaliyofunuliwa na Yesu Kristo. Kristo alipata ufunuo huu kutoka kwa Mungu, kusudi awaonyeshe watumishi wake mambo yanayopaswa kutokea kisha kidogo. Kristo alimutuma malaika wake kwa kumujulisha mutumishi wake Yoane mambo yale.


Naye Yoane alishuhudia kwamba mambo yote aliyoona yanaelekea Neno la Mungu na ukweli ulioshuhudiwa na Yesu Kristo.


Ni mimi Yoane ninayewaandikia ninyi makanisa saba munaokuwa katika jimbo la Azia. Ninawatakia neema na amani kutoka kwa Mungu anayekuwa, aliyekuwa na anayekuja, na kutoka kwa roho saba wanaokuwa mbele ya kiti chake cha kifalme,


Hivi akatupatia ufalme wa kikuhani kusudi tumutumikie Mungu Baba yake. Yesu Kristo atukuzwe na kuwa na uwezo kwa milele na milele. Amina.


Wakati watakapomaliza kutoa huo ushuhuda wa Mungu, yule nyama wa ajabu anayetoka katika kuzimu atapigana vita nao, naye atawashinda na kuwaua.


Wandugu zetu wamemushinda kwa nguvu ya damu ya Mwana-Kondoo na kwa njia ya ukweli walioshuhudia. Wao walikubali kutoa maisha yao mpaka kufa.


Yule nyoka akamukasirikia yule mwanamuke na kwenda kufanya vita na wazao wake wengine; ndio wale wanaoshika amri za Mungu na kufuata ukweli ulioshuhudiwa na Yesu Kristo.


Mutu yule aliyekusudiwa kuwa mufungwa, atafungwa; na yule aliyekusudiwa kuuawa kwa upanga, atauawa kwa upanga. Kwa sababu hiyo, watu wa Mungu wanapaswa kuwa wavumilivu na wenye imani.”


Kwa sababu hiyo, watu wa Mungu wanaoshika amri za Mungu na kumwamini Yesu wanapaswa kuwa wavumilivu.


Nikaanguka mbele yake kusudi nimwabudu, lakini akaniambia: “Angalia, usifanye vile! Kwa maana mimi ni mutumishi kama vile wewe na wandugu zako wanaoshika ukweli ulioshuhudiwa na Yesu. Ni Mungu ndiye unayepaswa kumwabudu! Maana ukweli ambao Yesu alishuhudia, ndio uwezo unaowaongoza manabii.”


Kisha nikaona viti vya kifalme na watu waliokuwa wakiikaa juu yao, wakapewa uwezo wa kuhukumu. Nikaona vilevile roho za wale waliochinjwa kwa sababu ya kutangaza ukweli ulioshuhudiwa na Yesu na Neno la Mungu. Watu wale hawakumwabudu yule nyama wa ajabu, wala sanamu yake, wala hawakupigwa chapa yake juu ya paji za nyuso zao, au juu ya mikono yao. Nao wakafufuka na kutawala pamoja na Kristo muda wa miaka elfu moja.


Kufuatana na vile ulivyojichunga katika uvumilivu sawa nilivyokuagiza, mimi vilevile nitakuchunga na hasara wakati itakapokuja katika dunia yote kwa kuwajaribu wakaaji wake.


Wakati Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa tano, nikaona chini ya mazabahu, roho za watu waliouawa kwa sababu ya kutangaza Neno la Mungu na kwa sababu ya ushuhuda wao.


Nami nikamujibu: “Bwana wangu wewe ndiwe unayejua.” Naye akaniambia: “Hawa ndio wanaotoka katika mateso makubwa. Wamesafisha kanzu zao na kuzifanya kuwa nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ