Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Ufunuo 1:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Naye Yoane alishuhudia kwamba mambo yote aliyoona yanaelekea Neno la Mungu na ukweli ulioshuhudiwa na Yesu Kristo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Ufunuo 1:2
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yoane akatoa ushuhuda huu: “Nimemwona Roho akishuka juu yake toka mbinguni kwa mufano wa njiwa na kukaa juu yake.


Wale watu wote waliokuwa pamoja na Yesu wakati alipomwita Lazaro toka ndani ya kaburi na kumufufua walishuhudia mambo yaliyofanyika.


Mutu aliyeona mambo hayo ndiye anayeyashuhudia, nao ushuhuda wake ni wa kweli. Na anajua kama anasema ukweli, kusudi mupate kuamini vilevile.


Ni huyu huyu mwanafunzi ndiye aliyeshuhudia mambo hayo na kuyaandika; nasi tunajua kwamba ushuhuda wake ni wa kweli.


Kweli, kweli ninakuambia: tunasema maneno tunayojua na kushuhudia maneno tuliyoona, lakini ninyi hamutaki kupokea ushuhuda wetu.


Kwa maana utatoa ushuhuda wake kwa watu wote, utasema juu ya mambo yale uliyoona na kuyasikia.


Lakini sasa inuka usimame wima. Nimekutokea kusudi nikuweke kuwa mutumishi wangu. Wewe utatoa ushuhuda juu yangu; utawaelezea watu mambo uliyoona leo na yale nitakayokuonyesha nyuma.


Kwa maana sisi hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo tuliyoyaona na kuyasikia.”


Ile inatokana na vile ujumbe juu ya Kristo umehakikishwa kwa nguvu kati yenu,


Wandugu zangu, wakati nilipokuja kwenu kuwapasha habari ya siri ya Mungu, sikutumia maneno magumu wala hekima ya dunia.


Tunawaandikia ninyi juu ya Neno la uzima, lililokuwa tangia mwanzo. Sisi tulilisikia, tuliliona kwa macho yetu wenyewe, tuliliangalia na kuligusa kwa mikono yetu wenyewe.


Na sisi tumeona na kushuhudia kwamba Baba amemutuma Mwana wake kuwa Mwokozi wa dunia.


Watu wote wameshuhudia Demetrio vizuri; hakika ukweli wenyewe unahakikisha jambo lile. Sisi vilevile tunamushuhudia, nawe unajua kwamba ushuhuda wetu ni wa kweli.


ikisema: “Andika katika kitabu mambo unayoona, na ukitume kwa makanisa ya miji saba: Efeso, Smurna, Pergamo, Tuatera, Sardi, Filadelfia na Laodikia.”


Basi uandike mambo unayoona, na mambo yanayokuwa sasa na yale yatakayotokea nyuma.


Mimi ni ndugu yenu Yoane. Kwa njia ya kuungana na Yesu, ninashirikiana nanyi katika mateso, katika ufalme wake na katika kuvumilia. Mimi nilikuwa nimepelekwa katika kisanga kinachoitwa Patimo, kwa sababu nilihubiri Neno la Mungu na ukweli ulioshuhudiwa na Yesu.


Wandugu zetu wamemushinda kwa nguvu ya damu ya Mwana-Kondoo na kwa njia ya ukweli walioshuhudia. Wao walikubali kutoa maisha yao mpaka kufa.


Yule nyoka akamukasirikia yule mwanamuke na kwenda kufanya vita na wazao wake wengine; ndio wale wanaoshika amri za Mungu na kufuata ukweli ulioshuhudiwa na Yesu Kristo.


Kisha nikaona viti vya kifalme na watu waliokuwa wakiikaa juu yao, wakapewa uwezo wa kuhukumu. Nikaona vilevile roho za wale waliochinjwa kwa sababu ya kutangaza ukweli ulioshuhudiwa na Yesu na Neno la Mungu. Watu wale hawakumwabudu yule nyama wa ajabu, wala sanamu yake, wala hawakupigwa chapa yake juu ya paji za nyuso zao, au juu ya mikono yao. Nao wakafufuka na kutawala pamoja na Kristo muda wa miaka elfu moja.


Ninawatakia ninyi wote neema kutoka kwa Bwana Yesu. Amina.


Wakati Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa tano, nikaona chini ya mazabahu, roho za watu waliouawa kwa sababu ya kutangaza Neno la Mungu na kwa sababu ya ushuhuda wao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ