Tito 3:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
14 Inafaa watu wetu vilevile wajifunze kuzidi kutenda mema kusudi wapate kutoa musaada kwa ajili ya mahitaji ya kweli. Na hivi maisha yao yatakuwa yenye mafaa.
na kuwapa wale wanaoomboleza katika Sayuni taji la maua pahali pa majivu juu ya kichwa, mafuta ya kuangarisha kwa furaha pahali pa maombolezo, nguo ya sifa pahali pa moyo muzito. Nao wataitwa miti ya mialo ya haki, Yawe aliyopanda kuonyesha utukufu wake.
Akaona muti wa tini pembeni ya njia, akaenda karibu nao, lakini hakuona kitu juu yake isipokuwa majani matupu. Halafu Yesu akaulaani muti ule akisema: “Wewe usitoe tena matunda tangu leo hata milele!” Na pale pale muti ule ukakauka.
Ninyi hamukunichagua mimi, lakini ni mimi niliyewachagua ninyi. Nami nimewatuma muende kuzaa matunda yasiyokuwa na mwisho. Kwa hiyo Baba atawapa chochote munachoomba kwa jina langu.
Katika mambo hayo yote niliyofanya, nimewaonyesha mufano kwamba tunapaswa kusumbuka vile na kazi kwa kuwasaidia wasiojiweza, tukikumbuka maneno haya Bwana Yesu mwenyewe aliyosema: ‘Ni heri kutoa kuliko kupewa.’ ”
Hivi, mutaweza kuishi sawa Bwana anavyotaka na kumupendeza katika mambo yote. Kwa njia hiyo mutafikia kufanya matendo mema ya kila namna na kuzidi kumujua Mungu.
Wandugu, munakumbuka namna tulivyosumbuka na kazi ngumu. Wakati tulipowahubiria Habari Njema ya Mungu, tulitumika muchana na usiku kusudi tusimulemee hata mutu mumoja kati yenu.
Neno hilo ni la kuaminiwa. Ninataka uyatilie maneno hayo mukazo, kusudi watu walioamini Mungu wajitolee kwa kuzidi kutenda mema. Jambo hilo ni zuri na lenye mafaa kwa watu.