Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Tito 3:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Inafaa watu wetu vilevile wajifunze kuzidi kutenda mema kusudi wapate kutoa musaada kwa ajili ya mahitaji ya kweli. Na hivi maisha yao yatakuwa yenye mafaa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Tito 3:14
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

na kuwapa wale wanaoomboleza katika Sayuni taji la maua pahali pa majivu juu ya kichwa, mafuta ya kuangarisha kwa furaha pahali pa maombolezo, nguo ya sifa pahali pa moyo muzito. Nao wataitwa miti ya mialo ya haki, Yawe aliyopanda kuonyesha utukufu wake.


Akaona muti wa tini pembeni ya njia, akaenda karibu nao, lakini hakuona kitu juu yake isipokuwa majani matupu. Halafu Yesu akaulaani muti ule akisema: “Wewe usitoe tena matunda tangu leo hata milele!” Na pale pale muti ule ukakauka.


Kila muti usiozaa matunda mazuri unakatwa na kutupwa katika moto.


Ninyi hamukunichagua mimi, lakini ni mimi niliyewachagua ninyi. Nami nimewatuma muende kuzaa matunda yasiyokuwa na mwisho. Kwa hiyo Baba atawapa chochote munachoomba kwa jina langu.


Kama mukizaa matunda mengi, Baba yangu atatukuzwa, na hivi mutakuwa kweli wanafunzi wangu.


Naye akakaa na kutumika pamoja nao, kwa maana wote walikuwa wafundi wa kutengeneza hema.


Katika mambo hayo yote niliyofanya, nimewaonyesha mufano kwamba tunapaswa kusumbuka vile na kazi kwa kuwasaidia wasiojiweza, tukikumbuka maneno haya Bwana Yesu mwenyewe aliyosema: ‘Ni heri kutoa kuliko kupewa.’ ”


Muwasaidie watu wa Mungu katika mahitaji yao na muwakaribishe wageni.


Basi nitakapomaliza kazi ile na kuwafikishia mali iliyokusanywa, nitapitia kwenu, nikiwa katika safari yangu ya kwenda Spania.


Yule aliyekuwa akiiba, asiibe tena, lakini ajikaze kufanya kazi peke yake kwa usawa kusudi apate kuwasaidia wakosefu.


Maisha yenu yatajazwa matendo ya haki ambayo Yesu Kristo anayowajalia, kwa ajili ya utukufu na sifa ya Mungu.


Hata wakati wote nilipokuwa Tesalonika, mulinitumia musaada mara nyingi juu ya mahitaji yangu.


Sitaki kusema kwamba ninatafuta tu kupokea zawadi, lakini ninataka faida iongezwe kwa upande wenu.


Hivi, mutaweza kuishi sawa Bwana anavyotaka na kumupendeza katika mambo yote. Kwa njia hiyo mutafikia kufanya matendo mema ya kila namna na kuzidi kumujua Mungu.


Wandugu, munakumbuka namna tulivyosumbuka na kazi ngumu. Wakati tulipowahubiria Habari Njema ya Mungu, tulitumika muchana na usiku kusudi tusimulemee hata mutu mumoja kati yenu.


Sisi hatukukula chakula cha mutu kwa bure, lakini tulitumika na kuchoka sana. Tulitumika muchana na usiku kusudi tusilemee hata mutu mumoja kati yenu.


Ufundishe maneno ya kweli watu wasiyoweza kubishia, hata wale wanaokupinga wapate haya kwa kukosewa na neno baya la kusema juu yetu.


Neno hilo ni la kuaminiwa. Ninataka uyatilie maneno hayo mukazo, kusudi watu walioamini Mungu wajitolee kwa kuzidi kutenda mema. Jambo hilo ni zuri na lenye mafaa kwa watu.


Kwa maana mukiwa na tabia hizi zote kwa uwingi, zitawawezesha kutumika na kuzaa matunda hata mupate kumujua Bwana wetu Yesu Kristo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ