Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Tito 3:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Kwa maana unajua kwamba mutu kama huyo amepotoka, na zambi zake zinamuhukumu yeye mwenyewe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Tito 3:11
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yule bwana akamujibu: ‘Wewe mutumishi mubaya! Nitakuhukumu kufuatana na maneno yako. Ulijua kama mimi ni mutu mugumu, ninayetafutia nafasi nisipowekea na kuvuna nafasi nisipopanda.


Lakini Wafarisayo na walimu wakubwa wa Sheria walikataa mupango wa Mungu juu yao, na kukataa kubatizwa na Yoane.)


Anayemwamini Mwana hahukumiwi, lakini asiyemwamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakumwamini Mwana wa pekee wa Mungu.


Halafu Paulo na Barnaba wakawaambia bila woga: “Ilitupasa kwanza kuhubiri Neno la Mungu kwenu. Lakini kwa kuona mumelikataa na kujihesabu ninyi wenyewe kwamba uzima wa milele haufai kwenu, basi tunashugulika na watu wa mataifa mengine.


Tumesikia kwamba watu fulani waliotoka huku kwetu pasipo ruhusa yetu wamewasumbua ninyi na maneno na kuwatia katika wasiwasi.


Basi tunajua kama maneno yote yanayosemwa na Sheria, yanawaelekea wale wanaolazimishwa kutii Sheria, kusudi mutu yeyote asikuwe na namna ya kujitetea, na dunia nzima ipaswe kuhukumiwa na Mungu.


Uwakumbushe watu maneno hayo yote na kuwaonya wazi mbele ya Mungu waache kubishana juu ya maneno. Mabishano hayana faida kwa maana yanawapoteza wale wanaoyasikia.


Inafaa kuwanyamazisha watu hao kwa sababu wanapotosha jamaa nzima kwa kufundisha mambo yasiyofaa wakitafuta kupata mali kwa njia mbaya.


Na zaidi ya ile hawatafuata hadisi za uongo za Kiyuda wala maagizo ya watu waliopotoka mbali na ukweli.


Kwa maana tukifanya zambi kwa makusudi tukisha kutambua waziwazi ukweli, hakuna tena sadaka ingine inayoweza kutolewa kwa ajili ya usamehe wa zambi zetu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ