Basi wandugu zangu wapenzi, musimame imara bila kutikisika. Muendelee kumutumikia Bwana siku zote, mukijua kwamba masumbuko munayopata kwa ajili ya Bwana hayatapita bure.
Kwa maana sisi ni viumbe vya Mungu, na kwa kuungana kwetu na Yesu Kristo, alituumba kusudi tuishi maisha ya matendo mema, ambayo Mungu alitutayarishia tangu mbele tupate kuyatenda.
Naye mutu atakayetenda kwa kiburi bila kutii kuhani aliyewekwa hapo kwa kumutumikia Yawe, Mungu wenu, au mwamuzi, mutu huyo atauawa. Ndivyo mutakavyokomesha uovu kati yenu.
Hivi, mutaweza kuishi sawa Bwana anavyotaka na kumupendeza katika mambo yote. Kwa njia hiyo mutafikia kufanya matendo mema ya kila namna na kuzidi kumujua Mungu.
Kama ukiwaelezea waziwazi wandugu maneno hayo, utakuwa mutumishi mwema wa Kristo Yesu, mwenye kukulishwa kiroho na maneno ya imani na mafundisho mazuri uliyoshika kabisa.
Sherti ajulikane kwa matendo yake mema. Anapaswa kuwa mutu aliyeadibisha watoto wake vizuri, aliyekaribisha wageni, aliyewapokea watu wa Mungu akiwanawisha miguu, aliyewasaidia wenye taabu na aliyejitolea kwa kutenda mema ya kila namna.
Uwakumbushe watu maneno hayo yote na kuwaonya wazi mbele ya Mungu waache kubishana juu ya maneno. Mabishano hayana faida kwa maana yanawapoteza wale wanaoyasikia.
Basi kama mutu atajitakasa kwa kujitenga na maovu hayo yote atakuwa chombo cha matumizi ya kipekee, kitakatifu cha mwenye nyumba na chenye mafaa kwake na kuwa tayari kwa kila kazi njema.
Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu, kusudi atukomboe toka uovu wote na kututakasa tupate kuwa watu wake wa pekee, watu wanaokuwa na hamu ya kufanya kazi nzuri.
Inafaa watu wetu vilevile wajifunze kuzidi kutenda mema kusudi wapate kutoa musaada kwa ajili ya mahitaji ya kweli. Na hivi maisha yao yatakuwa yenye mafaa.
Neno hilo ni la kuaminiwa. Ninataka uyatilie maneno hayo mukazo, kusudi watu walioamini Mungu wajitolee kwa kuzidi kutenda mema. Jambo hilo ni zuri na lenye mafaa kwa watu.
awakamilishe katika kila tendo jema kusudi mupate kutimiza mapenzi yake; yeye atimize ndani yetu yale yanayomupendeza, kwa njia ya Yesu Kristo. Yesu atukuzwe milele na milele. Amina.
Ijapokuwa mumekwisha kujua kabisa mambo haya yote, ninataka kuwakumbusha namna Bwana alivyowaokoa Waisraeli kutoka katika inchi ya Misri, lakini kisha, akawaangamiza wale waliokataa kuamini.