Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Tito 1:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Anapaswa kushika Neno la kweli linalolingana na mafundisho yetu. Hivi ataweza kuwaonya watu kwa njia ya mafundisho ya kweli na kuwashinda wale wanaomupinga.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Tito 1:9
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akamwambia Shetani: “Umemwona vizuri mutumishi wangu Yobu? Katika dunia hakuna mwingine anayekuwa kama yeye. Yeye ni mutu mukamilifu, wa usawa, mwenye kumwogopa Mungu na mwenye kuepukana na uovu. Yeye anadumu katika ukamilifu, ingawa wewe umenisukuma nimwangamize bure.”


Ninashikilia haki yangu, wala sitaiacha; katika zamiri yangu sina cha kunihukumu katika maisha yangu.


Nunua ukweli, wala usiuuzishe; nunua hekima, mafundisho na akili.


kwa maana alibishana na Wayuda mbele ya watu wote na kuwashinda kabisa. Aliwaonyesha kwa njia ya Maandiko Matakatifu kwamba Yesu ndiye Kristo.


Lakini kama wote wakitabiri, na kama mutu mumoja asiyeamini au asiyeelewa kitu anaingia, atapata uhakikisho kutokana na maneno ya hao wote. Naye atahukumiwa kufuatana na yote aliyosikia na


Lakini muchunguze kila jambo na kushika lile linalokuwa jema.


Basi wandugu, musimame imara na mushike mafundisho yetu tuliyowatolea, ikiwa kwa mahubiri au kwa barua yetu.


Sheria imewekwa kwa ajili ya waasherati, wanaume wanaozini wao kwa wao, wenye kuuzisha watu, wasema uongo, wale wanaofanya viapo vya uongo na kwa ajili ya wote wanaofanya matendo yanayokuwa umbalimbali na mafundisho ya kweli.


Neno hili ni la kuaminiwa nalo linastahili kukubaliwa kabisa: Kristo Yesu alikuja katika dunia kwa kuokoa wenye zambi. Na mimi ni wa kwanza mwenye zambi kati yao,


ukichunga imani yako na kuwa na zamiri safi. Watu wamoja wamekataa kuwa na zamiri hata wamepoteza imani yao.


Neno hilo ni la kuaminiwa, nalo linastahili kukubaliwa kabisa.


Kama mutu akifundisha mafundisho mengine, naye hakubali maneno ya kweli ya Bwana wetu Yesu Kristo wala mafundisho yanayolingana na dini yetu,


Ushike maneno ya kweli niliyokufundisha, yapate kuwa mufano kwako. Ushikamane na imani na upendo unaokuwa nao kwa njia ya kuungana kwako na Kristo Yesu.


Wewe umesikia mafundisho niliyotoa mbele ya washuhuda wengi. Nawe sasa uyafundishe kwa watu waaminifu watakaoweza vilevile kuyatoa kwa watu wengine.


Anapaswa kuwaonya kwa upole wale wanaopingana naye; kwa maana labda Mungu anaweza kuwajalia hata wapate kugeuka toka zambi na kutambua ukweli.


Lakini wewe ushikamane na mambo yale uliyofundishwa na kuyaamini kabisa. Unajua ni nani aliyekufundisha.


Maana kutakuja wakati watu watakapokataa kusikiliza mafundisho ya kweli, lakini watafuata tamaa zao wenyewe wakijitafutia walimu wengi kwa kuwafundisha mambo yale wanayotamani kusikia.


Inafaa kuwanyamazisha watu hao kwa sababu wanapotosha jamaa nzima kwa kufundisha mambo yasiyofaa wakitafuta kupata mali kwa njia mbaya.


Lakini kwa ngambo yako, ufundishe maneno yale yanayolingana na mafundisho ya kweli.


Wapendwa wangu, wakati nilipokuwa nikifanya bidii sana ya kuwaandikia juu ya wokovu tunaoshiriki wote pamoja, nikaona sherti niwaandikie na kuwaonya mupate kutetea imani ile Mungu aliyotoa mara moja tu kwa watu wake.


Lakini ninawaomba tu mushikamane na kile munachokuwa nacho mpaka nitakapokuja.


Ninakuja upesi. Shika sana kile unachokuwa nacho, kusudi mutu yeyote asinyanganye taji yako ya ushindi.


Basi ukumbuke mafundisho uliyopokea na yale uliyosikia. Uyashike na kugeuka toka zambi zako. Kama usipokesha, nitakuja kama mwizi, wala hautajua saa nitakapokuja kwako.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ