Mutangaze na kusema habari zenu. Mufanye shauri pamoja! Ni nani aliyetangaza zamani matukio ya sasa? Ni nani aliyesema mambo haya zamani? Haikukuwa mimi Yawe? Hakuna Mungu mwingine isipokuwa mimi! Mimi ni Mungu wa haki na mwokozi; hakuna mwingine isipokuwa mimi.
Halafu wafalme hao wawili wataikaa kwa meza pamoja, lakini kila mumoja anamuwazia mwenzake uovu, na kudanganyana. Lakini hawatafanikiwa, maana wakati uliopangwa utakuwa bado haujatimia.
Muda wa miaka saba mara makumi saba umewekwa kwa ajili ya watu wako na juu ya muji wako mutakatifu kwa kumaliza makosa, kukomesha zambi, kusamehe uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri juu ya maono na unabii na kupakaa mafuta katika Pahali Patakatifu Sana.
Kutokana na mutu mumoja, yeye aliumba watu wa mataifa yote kusudi waishi katika dunia yote. Aliwapangia nyakati na kukata mipaka ya inchi wanayopaswa kukaa ndani yake.
kwa njia ya uwezo wa vitambulisho na maajabu, na kwa uwezo wa Roho Mutakatifu. Hivi tokea Yerusalema mpaka kufika katika jimbo la Iliriko nimehubiri fasi zote Habari Njema ya Kristo.
Mungu asifiwe! Yeye yuko na uwezo wa kuwaimarisha katika imani juu ya Habari Njema ninayotangaza kwa kuhubiri ujumbe juu ya Yesu Kristo, kufuatana na ufunuo wa siri iliyofichwa tangia zamani za kale na kale.
Ingekuwa nimechagua kazi hii kwa mapenzi yangu mwenyewe, ningeweza kungojea kupokea mushahara. Lakini kwa kuwa ni muzigo niliopewa, inanipasa kuitimiza.
Lakini, inawapasa ninyi kuendelea na musingi imara katika imani, musitikiswe na kupoteza lile tumaini mulilopata wakati muliposikia Habari Njema. Mimi Paulo nimewekwa kuwa mutumishi wa kuhubiri Habari Njema ile iliyokwisha kutangazwa kwa watu wote katika dunia.
Habari Njema ile inatoa matunda na kuenea katika dunia yote sawa vile ilivyofanya kwenu tangu siku ile muliposikia wakisema juu ya neema ya Mungu na kupata kuitambua inavyokuwa kweli.
Lakini siku zote tunasema vile Mungu anavyotaka, kwa maana yeye aliamua kwamba tunastahili, akatupatia kazi ya kuhubiri Habari Njema yake. Sisi hatutafuti kuwapendeza watu, lakini tunataka kupendeza Mungu, anayejua siri za mioyo yetu.
Lakini Bwana alinisaidia, akanitia nguvu nipate kuitangaza Habari Njema kwa ukamilifu kusudi watu wa mataifa mengine wapate kuisikia. Nami nikaokolewa toka katika kinywa cha simba.
na kuiba vitu vyao. Lakini wajionyeshe kila mara kuwa waaminifu kamili, kusudi wapate kuheshimisha mafundisho juu ya Mungu Mwokozi wetu katika mambo yote.