Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Tito 1:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Na hata mumoja wa manabii wao wenyewe, Mukrete, alisema: “Wakrete ni wasema uongo siku zote, nyama wabaya, wavivu na walafi.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Tito 1:12
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

maana ‘kwa uwezo wake tunaishi, tunatenda na kuendelea kuwa.’ Ni sawa na maneno ya watunga mashairi wamoja wa kwenu waliosema: ‘Sisi vilevile tuko watoto wake.’


kati yao kuna Wayuda na watu waliofuata dini ya Kiyuda, na kuna watu wa inchi ya Krete na ya Arabia. Hata hivi tunawasikia hawa wote wakisema habari za matendo makubwa ya Mungu katika luga zetu za kuzaliwa!”


Na kwa sababu kivuko kile hakikukuwa na nafasi zuri ya kukaa wakati wa baridi kali, watu wengi kati yetu wakakubaliana kuondoka kule, kusudi ikiwezekana wafike Foinike, na kupitishia wakati wa baridi kali kule. Foinike ni kivuko kimoja kinachokuwa katika kisanga cha Krete, kinachoelekea upande wa kaskazini-magaribi na wa kusini-magaribi.


Upepo usiokuwa mukali ulipoanza kuvuma tokea kusini, wakazani kwamba wataweza tu kutimiza sawa walivyokuwa wamekusudia. Wakapandisha nanga na kuendelea pembenipembeni karibu sana na Krete.


Tukasafiri polepole muda wa siku nyingi na kwa shida sana tukafika karibu na muji Kinido. Na kwa sababu upepo ulituzuiza kuendelea mbali ngambo ile, tukapita upande wa kusini wa kisanga cha Krete, kuelekea Salmone.


Kwa maana watu wa namna hii hawamutumikii Bwana wetu Kristo, lakini wanatumikia tu tumbo yao wenyewe. Tena kwa maneno yao matamu na ya kujipendekeza wanadanganya watu wasiokuwa na makosa.


Mwisho wao ni uharibifu, sababu mungu wao ni kushibisha tumbo zao. Wanajivuna kwa kufanya mambo ya kuwafezehesha. Nayo mafikiri yao ni juu ya vitu vya dunia hii.


Wanadanganywa na watu wenye uongo na wanafiki wenye zamiri iliyokufa, iliyoharibika kabisa kama vile imeteketezwa kwa moto.


Nimekuacha katika kisanga cha Krete kusudi upate kutengeneza maneno yaliyobaki na kusimika wazee katika kanisa ndani ya kila muji, ukifuata maagizo niliyokutolea:


Walimu hawa wa uongo ni kama nyama wasiokuwa na akili ambao wanazaliwa tu kwa kunaswa na kuchinjwa. Wao wanasema vibaya juu ya mambo yote wasiyojua. Wataangamizwa kufuatana na ubaya wao wenyewe.


Wameacha njia ya kweli na kupotoka wakifuata njia ile Balama, mwana wa Beori, aliyofuata. Huyu alipenda kupata mali kwa njia isiyokuwa ya haki,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ