Hanameli mwana wa baba yako mudogo Salumu atakuja kwako na kusema: Nunua shamba langu linalokuwa kule Anatoti, maana wewe ni ndugu yangu kabisa, nawe uko na haki ya kulikomboa.
Mutu yule aliitwa Elimeleki na muke wake aliitwa Naomi. Watoto wao wawili wanaume, mumoja aliitwa Malona na mwingine Kiliona. Mutu yule na jamaa yake walikuwa wa kabila la Efuraimu kule Betelehemu katika Yuda. Walikwenda katika inchi ya Moabu, wakakaa kule.