Warafiki watatu wa Yobu walisikia juu ya hasara zote zilizomupata Yobu, wakaamua kwa pamoja waende kumupa pole na kumufariji. Majina yao ni: Elifasi kutoka inchi ya Temani, Bildadi wa inchi ya Suhi na Zofari wa inchi ya Namati.
Kwa hiyo, musikilize mupango ambao mimi Yawe nimepanga juu ya Edomu pamoja na mambo niliyokusudia kuwafanyia wakaaji wa Temani: Hakika, watoto wao wadogo watakokotwa na kukamatwa; kweli kutakuwa mushangao mukubwa katika makao yao!
Adui atapanda juu na kuruka kama tai na kutandaza mabawa yake juu ya Bosira. Siku hiyo moyo wa mashujaa wa Edomu utakuwa kama vile moyo wa mwanamuke anayezaa.
basi, Bwana wetu Yawe anasema: Nitanyoosha mukono juu ya inchi ya Edomu kwa kuwaazibu na kuwaua watu wote na nyama. Nitaifanya kuwa ukiwa kutoka muji wa Temani mpaka muji wa Dedani. Watu wa inchi hiyo watauawa kwa upanga.
Kama wizi au wanyanganyi wangekufikia usiku, si wao wangekuiba tu vitu wanavyokuwa navyo lazima? Ikiwa wavunaji wa zabibu wangekufikia, si wangekuachia sehemu ndogo tu? Lakini wewe, waadui zako wamekuangamiza kabisa.
musipigane nao kwa sababu sitawapa sehemu yoyote ya inchi yao. Sitawapa hata pahali padogo pa kukanyaga. Inchi hiyo ya milima ya Seiri nimewapa wazao wa Esau ikuwe mali yao.