Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 9:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Walawi, ni kusema Yesua, Kadimieli, Bani, Hasabuea, Serebia, Hodia, Sebania na Petahia, wakawaambia watu: Musimame na kumusifu Yawe, Mungu wenu. Mumusifu milele na milele! Na watu wakasifu jina lako tukufu, ambalo linatukuka kuliko baraka na sifa zote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 9:5
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha, Solomono akawaelekea Waisraeli wote walipokuwa wakisimama, akawabariki,


akasema: “Atukuzwe Yawe, Mungu wa Israeli, maana kwa nguvu yake ametimiza ahadi yake aliyomupa baba yangu Daudi, akisema:


Kisha Solomono alisimama kwenye mazabahu ya Yawe, mbele ya Waisraeli wote, aliinua mikono yake juu,


“Lakini, ee Mungu, kweli utakaa katika dunia? Ikiwa hata mbingu zenyewe wala mbingu za juu sana hazikutosha, namna gani nyumba hii ambayo nimeijenga itakutoshelea?


Asifiwe Yawe, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele! Kisha watu wote wakasema: “Amina!” Wakamusifu Yawe vilevile.


Ukubwa ni wako, ee Yawe, una nguvu, utukufu, ushindi na mamlaka. Vyote vinavyokuwa mbinguni na katika dunia ni vyako. Ee Yawe, ufalme ni wako, nawe umetukuzwa, uko mukubwa juu ya vitu vyote.


Sasa, ee Mungu wetu, tunakushukuru na kusifu jina lako tukufu.


Kisha, mufalme Daudi akawaambia wote waliokusanyika: “Mumusifu Yawe, Mungu wenu.” Na wote waliokusanyika wakamutukuza Yawe, Mungu wa babu zao, wakainama mbele yake na kumwabudu Yawe na kumutolea mufalme Daudi heshima.


Wanaume wote wa Yuda, pamoja na wake zao na watoto wao, walikuwa wakisimama pale mbele ya Yawe.


Walawi na ukoo wa Kohati na Kora, wakasimama na kumusifu Yawe, Mungu wa Israeli, kwa sauti kubwa sana.


Wakaimba kwa kupokezana, wakimusifu na kumutukuza Yawe: “Yeye ni muzuri, wema wake kwa Waisraeli unadumu milele.” Watu wote walipaza sauti kwa nguvu zao zote, wakamusifu Yawe kwa sababu ya kuanza kujenga musingi wa nyumba ya Yawe.


Kuliwekwa daraja la Walawi; pale kulisimama Yesua, Bani, Kadimieli, Sebania, Buni, Serebia, Bani na Kenani. Wakamwomba kwa sauti kubwa Yawe, Mungu wao.


Ezra akaomba akisema: Wewe peke yako ndiwe Yawe! Ulifanya mbingu na jeshi lake lote, dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake, bahari na vyote vinavyokuwa ndani yake. Unavipatia uzima, na jeshi lote la mbinguni linakuabudu wewe.


akisema: Nilikuja uchi katika dunia, nitaondoka uchi katika dunia. Yawe amenipa, Yawe ametwaa. Jina la Yawe litukuzwe.


Ni nani anayeweza kutaja matendo ya Yawe? Ni nani anayeweza kumusifu kama anavyostahili?


Wimbo wa safari za kidini. Mukuje kumusifu Yawe, enyi watumishi wake wote, enyi wote munaotumikia ndani ya nyumba yake usiku.


Nitakutukuza kila siku; nitalisifu jina lako kwa milele na milele.


Nitasema juu ya utukufu na mamlaka yako, nitafikiri juu ya matendo yako ya ajabu.


Nitamusifu Yawe maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu muda wote nitakapoishi.


Ninamwambia Mungu: “Wewe ni Bwana wangu; sina uheri wowote isipokuwa wewe.”


Muimbe kwa ajili ya utukufu wa jina lake, mumusifu kwa utukufu!


Wote wasifu jina lake kubwa la kutisha. Yeye ni mutakatifu!


“Ewe Yawe, ni nani kati ya miungu anayelingana nawe? Ni nani aliyekuwa kama wewe unayekuwa mutakatifu mukubwa, unayetisha kwa matendo matukufu, unayetenda mambo ya ajabu?


“Mukono wako wa kuume, ee Yawe, unatukuka kwa nguvu; kwa mukono wako wa kuume, ee Yawe, unawaponda waadui.


akasema: Jina la Mungu litukuzwe milele na milele. Hekima na nguvu ni vyake.


Katika siku zile Yesu akasema: “Ee Baba, Mwenyeji wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo.


Yule Mungu aliyesema: “Mwangaza uangaze katika giza,” ndiye aliyeangaza ndani ya mioyo yetu, na kutuwezesha kufahamu utukufu wa Mungu unaongaa kwenye uso wa Kristo.


“Kama musipokuwa waangalifu kwa kushika maneno yote ya sheria hii iliyoandikwa katika kitabu hiki na musipoheshimu na kutukuza jina tukufu la kuogopesha la Yawe, Mungu wenu


Tumusifu Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa huruma yake kubwa ametupatia uzima mupya kwa njia ya kumufufua Yesu Kristo. Na kwa hiyo tumepata tumaini lenye uzima,


Malaika wa Yawe akamujibu: “Kwa nini unataka kujua jina langu? Ni la ajabu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ