Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 9:35 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

35 Hawakukutumikia katika ufalme wao, wala walipofurahia mema yako mengi uliyowajalia kwa wingi, katika inchi kubwa na yenye mboleo uliyowapa hawakuyaacha matendo yao maovu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 9:35
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakateka miji yenye kuta, wakatwaa inchi yenye utajiri, nyumba zenye vitu vingi vizuri, visima vilivyochimbwa, mashamba ya mizabibu na mizeituni pamoja na miti yenye matunda kwa wingi. Hivyo wakakula, wakashiba na kunenepa na kufurahia wema wako.


Wafalme wetu, wakubwa wetu, makuhani wetu na babu zetu hawakushika Sheria yako wala kujali amri zako na maonyo yako uliyowapa.


Nitakumbusha mema ya Yawe, sifa za Yawe, matendo yake yote kwetu, mambo mazuri aliyowatendea Waisraeli, rehema yake, na wingi wa wema wake.


Na watu wenu watakapouliza: Kwa nini Yawe, Mungu wetu, ametutendea mambo hayo yote? Wewe Yeremia utawajibu hivi: Ninyi mulimwacha Yawe, mukaitumikia miungu ya kigeni katika inchi yenu. Basi ndivyo mutakavyowatumikia watu wengine katika inchi isiyokuwa yenu.


Lakini wakaaji wake wameyaasi maagizo na masharti yangu, wakakuwa wabaya kuliko mataifa na inchi zinazowazunguka. Kweli, wameyakataa maagizo yangu na kuacha kuyafuata masharti yangu.


“Yawe, Mungu wenu aliwabariki katika kila njia, lakini ninyi hamukumutumikia kwa moyo wa furaha na shangwe.


Kwa hiyo mutawatumikia waadui zenu ambao Yawe atawatuma mbele yenu, kwa njaa, kiu na uchi, na ukosefu wa kila kitu. Atawafunga nira ya chuma mpaka awaangamize.


Watakapopatwa na hasara nyingi na taabu, wimbo huu utakuwa kama ushuhuda maana hautasahauliwa na wazao wao. Hata sasa, mbele sijawapeleka katika inchi niliyoapa kuwapa, ninajua mipango ambayo wanapanga.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ