Lakini Yawe aliwarehemu na kuwaonea huruma. Aliwaangalia kwa wema kwa sababu ya agano lake na Abrahamu, Isaka na Yakobo. Hakuwaangamiza wala hajawaachilia hata kidogo mpaka leo.
Mukimurudilia Yawe, wale ambao walipeleka wandugu zenu na watoto wenu kuwa wafungwa, watawahurumia na kuwaacha warudi katika inchi hii. Kwa maana Yawe, Mungu wenu, ni mwenye huruma na rehema, naye hatawageuzia mugongo ikiwa mutamurudilia.”
Wakakataa kutii; hawakukumbuka maajabu uliyofanya kati yao. Wakakuwa wagumu, wakajichagulia kiongozi wa kuwarudisha katika utumwa katika inchi ya Misri. Lakini wewe Mungu uko mwepesi kwa kusamehe, mwenye huruma na rehema, haukasiriki upesi, uko mwema sana. Haukuwatupilia
lakini wewe kwa rehema zako nyingi haukuwatupilia kule katika jangwa. Nguzo la wingu lililowaongoza muchana, wala nguzo la moto lililowaangazia katika njia usiku, havikuondoka.
Mupande, mupite katika mashamba yake ya mizabibu, muharibu kila kitu lakini musivimalize kabisa. Mukate matawi yake, kwa maana hayo si yangu mimi Yawe.