Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 9:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Lakini hawakukuwa waaminifu kwako. Wakakuasi, wakaacha sheria yako na kuwaua manabii waliowaonya kusudi wakurudilie wewe. Wakatenda zambi kubwa mbele yako.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 9:26
35 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wewe umetenda uovu mubaya zaidi kuliko waliotenda wale waliokutangulia. Wewe umenikasirikisha kwa kujitengenezea miungu mingine na sanamu za kufua, kisha umeniacha.


Hauna habari kwamba Yezebeli alipokuwa akiwaua manabii wa Yawe, mimi niliwatwaa manabii mia moja nikawaficha makumi tano tano katika pango, nikakuwa ninawapatia chakula na maji?


na wakati Yezebeli alipowaua manabii wa Yawe, Obadia aliwachukua manabii mia moja, akawaficha makumi tano tano ndani ya pango, akakuwa anawapelekea chakula na maji.


Naye akasema: “Ninaona uchungu na wivu, ee Yawe, Mungu wa majeshi, kwa sababu watu wa Israeli wamevunja agano lako, wakazibomoa mazabahu zako na kuwaua manabii wako kwa upanga; ni mimi tu niliyebaki, nami vilevile wananiwinda waniue!”


Halafu Yawe akasema kupitia kwa watumishi wake manabii:


“Kwa sababu mufalme amefanya mambo ya kuchukiza, mambo mabaya zaidi ya yale yaliyotendwa na Waamori waliomutangulia, akawasukuma watu wa Yuda vilevile watende zambi kwa kutumia sanamu zake,


Lakini wao waliendelea kuwachekelea wajumbe wa Mungu, wakayazarau maneno yake na kuwachekelea manabii wake mpaka kwa mwisho kasirani ya Yawe ikawaka juu ya watu wake hata hakukukuwa wa kuwaponyesha.


hata walipojitengenezea sanamu ya mwana-ngombe na kusema: “Huyu ndiye Mungu wetu aliyetutoa kutoka katika inchi ya Misri.” Wakakuchukiza sana


Ukawaonya kusudi warudilie Sheria yako, hata hivyo, kwa kiburi chao, wakaacha kutii amri zako. Wakaasi maagizo yako, ambayo kwa njia yake mutu akiyatii, ataishi. Wakakuwa wenye kiburi vilevile wakakuwa wagumu, na wakakataa kuwa watiifu.


Ukawavumilia kwa miaka mingi, na kuwaonya kwa njia ya roho wako kwa kupitia manabii wako; hata hivyo hawakusikiliza. Basi ukawaacha ukawatia katika mikono ya mataifa mengine.


Wewe unachukia maonyo, na maneno yangu haupendi kuyafuata.


Nawe utawajibu hivi: Babu zenu waliniacha. Wakafuata miungu mingine, wakaitumikia na kuiabudu. Waliniacha, wala hawakuzitii sheria zangu.


Niliwaazibu ninyi lakini ilikuwa bure, ninyi munakataa maonyo. Muliwateketeza manabii wenu kwa upanga kama simba mwenye uchu.


Niliwaleta katika inchi yenye mboleo, muyafurahie mazao yake na mema yake mengine. Lakini mulipofika tu, muliichafua inchi yangu; inchi niliyowapa ikuwe yenu, mukaifanya chukizo.


Nao walifika, wakaitwaa na kuirizi. Lakini wao hawakukusikiliza, wala hawakufuata sheria zako. Hawakutenda mambo uliyoamuru. Ndiyo maana utawafanya wapatwe na hasara hii.


Yeremia akawaambia watu: Enyi Wayuda muliobaki, Yawe aliwaambia musiende Misri. Mujue wazi kwamba leo nimewaonya kwamba


Tulikukosea na kukuasi, nawe haujatusamehe bado.


Lakini hata wazao wao hao waliniasi. Hawakufuata masharti yangu, hawakushika wala kutimiza maagizo yangu ambayo mutu akiyashika, ataishi. Walizikufuru Sabato zangu. Basi nikasema kwamba nitawamwangia kasirani yangu na kuitimiza hasira yangu juu yao kule katika jangwa.


Lakini wale walimaji wakawakamata wale watumishi. Wakamupiga mumoja, wakamwua mwingine na kumutupia mwingine mawe hata akakufa.


Ni nani kati ya manabii ambaye babu zenu walikosa kumutesa? Waliwaua wale waliotabiri zamani habari za kuja kwa Mwenye Haki. Na sasa mumemutoa na kumwua.


Aliwapa siagi na maziwa ya mifugo, mafuta ya wana-kondoo na kondoo dume, makundi ya mifugo ya Basani na mbuzi. Aliwapa ngano nzuri kabisa na divai mupya wakakunywa.


Watu wa usawa walinona, wakapiga mateke. Walinenepa sana, kisha wakamwacha Mungu aliyewaumba, wakazarau Mulima wa wokovu wao.


Waisraeli wakatenda tena uovu mbele ya Yawe, wakatumikia Mabali, Mastaroti, na miungu ya Aramu, ya Sidona, ya Moabu, ya Amoni na ya Wafilistini. Wakamwacha Yawe wala hawakumwabudu tena.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ