Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 9:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Ukawatunza katika jangwa kwa miaka makumi ine na hawakukosa kitu chochote; nguo zao hazikuchakaa wala miguu yao haikuvimba.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 9:21
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mumwabudu Yawe, enyi watakatifu wake, maana wenye kumwabudu hawakosewi kitu.


Waisraeli walikula mana kwa muda wa miaka makumi ine, mpaka walipofika katika inchi iliyofaa kwa kuishi, ni kusema mpaka walipovuka mupaka wa Kanana.


Enyi Waisraeli, wakati ule mulipokuwa kule katika jangwa kwa miaka makumi ine, muliniletea matoleo na sadaka hata mara moja?


na kuwavumilia katika jangwa kwa muda wa miaka makumi ine.


“Basi, mukumbuke jinsi Yawe Mungu wenu alivyowabariki ninyi katika kila jambo mulilofanya. Aliwatunza mulipokuwa munatangatanga katika jangwa hili kubwa. Amekuwa pamoja nanyi miaka hii yote makumi ine na hamukupungukiwa na kitu chochote.


Hamukukula mukate wala kunywa divai au kileo chochote. Na hivyo mutapata kujua kwamba Yawe ni Mungu wenu.


Mukumbuke jinsi Yawe, Mungu wenu, alivyowaongoza katika safari ndefu kupitia katika jangwa kwa muda wa miaka hiyo makumi ine, kusudi awanyenyekeze na kuwajaribu kusudi ajue yanayokuwa ndani ya mioyo yenu, na kama mungeshika amri zake au hapana.


Wakati huo wa miaka makumi ine nguo zenu hazikuchakaa, wala miguu yenu haikuvimba.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ