Ukawavumilia kwa miaka mingi, na kuwaonya kwa njia ya roho wako kwa kupitia manabii wako; hata hivyo hawakusikiliza. Basi ukawaacha ukawatia katika mikono ya mataifa mengine.
Waisraeli walipoona kitu kile wakashangaa, wakaulizana: “Nini hii?” Hawakujua kilikuwa kitu gani. Basi, Musa akawaambia: “Huu ni mukate ambao Yawe amewapa mukule.
Halafu Yawe akamwambia Musa: “Mimi nitawanyeshea mikate kutoka mbinguni. Kila siku watu watatoka na kukusanya chakula cha siku hiyo. Kwa njia hii nitawapima nione kama watafuata sheria zangu au hawatazifuata.
Angalia mimi nitasimama mbele yako juu ya jiwe la mulima wa Horebu, nawe utapiga lile jiwe na maji yatabubujika kutoka mule kusudi watu wote wapate kunywa.” Basi, Musa akafanya hivyo mbele ya wazee wa Waisraeli.
Hawatasikia tena njaa wala kuwa na kiu. Upepo wenye kuunguza wala jua havitawachoma, mimi niliyewahurumia nitawaongoza na kuwapeleka kwenye chemichemi za maji.
Nitashuka kule na kuzungumuza nawe; nitatwaa sehemu ya roho niliyokupa, niwape watu hao. Nao watabeba muzigo wa kuwatunza watu hawa pamoja nawe, kusudi usibebe muzigo huo peke yako.
Yesu akamujibu: “Kama ungejua kitu Mungu anachoweza kukupatia, na ni nani anayekuomba maji ya kunywa, wewe ndiwe ungemwomba, naye angekupa maji ya uzima.”
lakini yeyote atakayekunywa maji yale nitakayomupa, hatasikia kiu tena hata kidogo. Maji nitakayomupa yatakuwa ndani yake kama chemichemi inayotiririka maji ya uzima wa milele.”
Wandugu zangu, ninawasihi kwa ajili ya Bwana wetu Yesu Kristo na kwa ajili ya upendo unaoletwa na Roho wa Mungu, muungane nami kwa kuniombea kwa Mungu.