Sasa musikuwe wenye mioyo migumu kama babu zenu lakini mumutii Yawe. Mukuje katika Pahali Patakatifu pake Yerusalema, ambako ametakasa milele, mumwabudu Yawe, Mungu wenu, kusudi asiwakasirikie.
Sedekia alimwasi vilevile mufalme Nebukadneza aliyekuwa amemufanya aape kwa jina la Mungu kwamba hatamwasi. Alikuwa mupotovu sana na kufanya moyo mugumu, akakataa kumugeukia Yawe, Mungu wa Israeli.
Ulifanya miujiza na maajabu mbele ya Mufalme wa Misri, watumishi wake wote na watu wote wa inchi yake; maana ulijua kwamba waliwagandamiza babu zetu. Ukajipatia utukufu unaokuwa mpaka leo.
Ukawaonya kusudi warudilie Sheria yako, hata hivyo, kwa kiburi chao, wakaacha kutii amri zako. Wakaasi maagizo yako, ambayo kwa njia yake mutu akiyatii, ataishi. Wakakuwa wenye kiburi vilevile wakakuwa wagumu, na wakakataa kuwa watiifu.
Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Mimi nitaleta juu ya muji huu na juu ya vijiji vyote vinavyokuwa kandokando yake hasara zote nilizotangaza juu yake, kwa sababu wakaaji wake ni wenye mioyo migumu, nao wamekataa kusikia maneno yangu.
Enyi watu! Musikilize vile mimi Yawe ninavyosema: Nimekuwa kama vile jangwa au inchi yenye giza kubwa? Kwa nini basi watu wangu wanasema: Sisi tuko watu huru; hatutakurudilia!
Lakini wakaaji wake wameyaasi maagizo na masharti yangu, wakakuwa wabaya kuliko mataifa na inchi zinazowazunguka. Kweli, wameyakataa maagizo yangu na kuacha kuyafuata masharti yangu.
Heri wangekuwa siku zote na mawazo kama haya wakiniheshimu na kushika amri zangu! Mambo yao yote yangewaendekea vizuri, wao wenyewe na wazao wao milele.
Lakini muonyane kila siku kwa muda wote ambao lile neno “leo” linalotajwa lingali linatuelekea kusudi hata mumoja wenu asikuwe mugumu kwa kudanganywa na zambi.
Maandiko Matakatifu yanasema: “Leo ikiwa munasikiliza sauti ya Mungu, musifanye mioyo yenu kuwa migumu kama babu zenu walivyofanya wakati walipomwasi Mungu.”