Nehemia 9:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
15 Walipokuwa na njaa, ukawapa chakula kutoka mbinguni. Walipokuwa na kiu, ukawapa maji kutoka katika jiwe. Ukawaagiza kurizi inchi uliyokuwa umewaahidi.
Halafu Yawe akamwambia Musa: “Mimi nitawanyeshea mikate kutoka mbinguni. Kila siku watu watatoka na kukusanya chakula cha siku hiyo. Kwa njia hii nitawapima nione kama watafuata sheria zangu au hawatazifuata.
Angalia mimi nitasimama mbele yako juu ya jiwe la mulima wa Horebu, nawe utapiga lile jiwe na maji yatabubujika kutoka mule kusudi watu wote wapate kunywa.” Basi, Musa akafanya hivyo mbele ya wazee wa Waisraeli.
Nao walifika, wakaitwaa na kuirizi. Lakini wao hawakukusikiliza, wala hawakufuata sheria zako. Hawakutenda mambo uliyoamuru. Ndiyo maana utawafanya wapatwe na hasara hii.
Muangalie, Yawe, Mungu wenu, ameiweka inchi hii mbele yenu. Basi! Muende, muirizi kama vile Yawe, Mungu wa wazee wenu alivyowaambia. Musiogope wala musifazaike!’
Inchi hii yote nimeiweka mbele yenu. Basi, muende kutwaa inchi hiyo ambayo mimi Yawe niliapa kuwapa wazee wenu Abrahamu, Isaka, Yakobo na wazao wao.’ ”
Aliwazarau akawaacha muone njaa na kisha akawapa mana mukule, chakula ambacho hamukukijua, wala babu zenu hawajapata kukijua. Alifanya hivyo kusudi apate kuwafundisha kwamba mwanadamu haishi kwa mukate tu, lakini kwa kila neno Yawe analosema.