Wakati wote mutatii masharti, maagizo, sheria na amri ambazo niliandika kwa ajili yenu, siku zote mutakuwa waangalifu kwa kuzitenda. Musiiabudu miungu mingine,
Ezra akaondoka Babeli, yeye alikuwa mwandishi mwenye ujuzi mwingi sana katika Sheria ambayo Yawe, Mungu wa Israeli, alikuwa amemupatia Musa. Na kwa musaada wa Yawe, Mungu wake, mufalme alimupatia Ezra kila kitu alichohitaji.
Musa akawaambia: “Hii ndiyo amri ya Yawe. Kesho ni siku ya mapumziko. Ni Sabato takatifu ya Yawe. Basi, muende mupike au kuchemusha kile chakula munachohitaji leo na chakula kitakachobakia mukiweke mpaka kesho.”
Ingeteketea kama moto unavyochoma kichaka, kama vile moto unavyochemusha maji. Ukuje upate kuwajulisha waadui zako jina lako nayo mataifa yatetemeke mbele yako!
Tangu zamani hakuna aliyepata kusikia kwa masikio yake wala kumwona Mungu anayekuwa kama wewe, anayetenda mambo kama hayo kwa ajili ya wale wanaomutegemea!
Yawe alikuja kutoka mulima Sinai, alitutokea kutoka mulima Seiri, aliangaza kutoka mulima Parani. Alitokea kati ya maelfu ya wamalaika, na moto unaowaka katika mukono wake wa kuume.
Aliwafanya muisikie sauti yake kutoka mbinguni kusudi aweze kuwafundisha; na hapa katika dunia akawafanya muone moto wake mukubwa na kusikia maneno yake kutoka katikati ya moto huo.