Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 9:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Kule kwa mulima Sinai ulishuka toka mbinguni na kuzungumuza nao. Ukawapa maagizo safi, sheria za kweli, masharti mazuri na amri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 9:13
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati wote mutatii masharti, maagizo, sheria na amri ambazo niliandika kwa ajili yenu, siku zote mutakuwa waangalifu kwa kuzitenda. Musiiabudu miungu mingine,


Ezra akaondoka Babeli, yeye alikuwa mwandishi mwenye ujuzi mwingi sana katika Sheria ambayo Yawe, Mungu wa Israeli, alikuwa amemupatia Musa. Na kwa musaada wa Yawe, Mungu wake, mufalme alimupatia Ezra kila kitu alichohitaji.


Ee Yawe, wewe ni wa haki; na hukumu zako ni za usawa.


Kifungo cha neno lako ni ukweli, maamuzi yako yote ya haki yanadumu milele.


Ee Mungu, umetupatia kanuni zako kusudi tuzishike kwa uangalifu.


Musa akawaambia: “Hii ndiyo amri ya Yawe. Kesho ni siku ya mapumziko. Ni Sabato takatifu ya Yawe. Basi, muende mupike au kuchemusha kile chakula munachohitaji leo na chakula kitakachobakia mukiweke mpaka kesho.”


wakuwe tayari kwa kesho kutwa, maana siku hiyo ya tatu mimi Yawe nitashuka juu ya mulima Sinai mbele ya watu wote.


Yawe akamwambia Musa: Uwaambie Waisraeli: Mumejionea ninyi wenyewe kwamba nimeongea nanyi kutoka mbinguni.


Ingeteketea kama moto unavyochoma kichaka, kama vile moto unavyochemusha maji. Ukuje upate kuwajulisha waadui zako jina lako nayo mataifa yatetemeke mbele yako!


Tangu zamani hakuna aliyepata kusikia kwa masikio yake wala kumwona Mungu anayekuwa kama wewe, anayetenda mambo kama hayo kwa ajili ya wale wanaomutegemea!


Mungu amekuja kutoka jimbo la Temani, Mungu mutakatifu anakuja kutoka mulima Parani. Utukufu wake umeenea pote mbinguni, nayo dunia imejaa sifa zake.


Ikiwa kile ninachofanya ndicho nisichotaka, maana yake ninakubali ya kuwa Sheria ni nzuri.


Yawe alikuja kutoka mulima Sinai, alitutokea kutoka mulima Seiri, aliangaza kutoka mulima Parani. Alitokea kati ya maelfu ya wamalaika, na moto unaowaka katika mukono wake wa kuume.


Watu walikwisha kusikia sauti ya Mungu ikisema toka katikati ya moto, kama ninyi mulivyosikia, wakabaki wazima?


Aliwafanya muisikie sauti yake kutoka mbinguni kusudi aweze kuwafundisha; na hapa katika dunia akawafanya muone moto wake mukubwa na kusikia maneno yake kutoka katikati ya moto huo.


Wala hakuna taifa lingine lolote hata likuwe kubwa namna gani, lenye masharti na maagizo ya haki, kama hayo ambayo nimewafundisha siku hii ya leo.


Yawe alisema nanyi kinywa kwa kinywa huko kwenye mulima katikati ya moto.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ