Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 9:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Uligawanya bahari katikati mbele yao, nao wakapita katikati ya bahari, pahali pakavu. Lakini ukawatupa Wamisri waliowafuatilia kama jiwe zito ndani ya maji mengi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 9:11
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Aligeuza bahari kuwa inchi kavu, watu wakapita humo kwa miguu; kwa hiyo nasi tukashangilia.


Aligawanya bahari, akawapitisha ndani yake; aliyafanya maji yasimame kama ukuta.


Yawe atawapigania. Ninyi mutakaa kimya tu.”


Alikwamisha magurudumu ya magari yao, yakakuwa yakienda kwa shida sana. Halafu Wamisri wakasema: “Tuwakimbie Waisraeli! Yawe anawapigania Waisraeli mbele yetu.”


Lakini Waisraeli walipita katikati ya bahari pahali pakavu, kuta za maji zikiwa zimesimama upande wao wa kuume na wa kushoto.


Katika inchi ya Misri ulifanya maajabu, ukatenda miujiza, na unaendelea kufanya hivyo mpaka leo kati ya Waisraeli na katika mataifa mengine vilevile, jambo ambalo limekufanya ujulikane kila nafasi.


Wandugu zangu, ninataka mukumbuke kwamba babu zetu wote walisafiri wakiongozwa na wingu, nao wote walivuka katikati ya bahari Nyekundu kwa usalama.


Kwa njia ya imani, Waisraeli walivuka bahari Nyekundu kama vile ingekuwa katika inchi kavu. Lakini wakati Wamisri walipojaribu kufanya vile, walizama na kufa ndani ya maji.


Kisha malaika mumoja mwenye uwezo akanyanyua jiwe linalokuwa kama jiwe kubwa la kusagia. Akalitupa katika bahari akisema: “Ni hivi muji mukubwa wa Babeli utakavyotupwa kwa nguvu, nao hautaonekana tena.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ