Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 8:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Wakasoma vizuri toka kitabu cha Sheria ya Mungu na kuifafanua na watu wote waliweza kuielewa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 8:8
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye mufalme akaenda katika nyumba ya Yawe pamoja na watu wote wa Yuda na wakaaji wote wa Yerusalema, na makuhani pamoja na manabii, watu wote, wadogo kwa wakubwa. Basi, akawasomea maneno ya kitabu cha agano kilichopatikana katika nyumba ya Yawe.


Barua muliyonitumia imetafsiriwa na kusomwa mbele yangu.


Watu wote wakarudi kwao kwa kula na kunywa, wakifurahi na kuwagawanyia wengine chakula kwa sababu walielewa yote waliyotangaziwa.


Walawi hawa ndio walisaidia kuwaelewesha watu Sheria: Yesua, Bani, Serebia, Yamini, Akubu, Sabetayi, Hodia, Maasea, Kelita, Azaria, Yozabadi, Hanani na Pelaya; na kila mumoja akiwa akisimama pale alipokuwa.


Watu waliposikia Sheria, wakaguswa ndani ya mioyo yao, halafu wote wakaanza kulia. Hivyo Nehemia aliyekuwa mutawala na Ezra kuhani na mwandishi, pamoja na Walawi waliofundisha watu wakawaambia watu wote: “Siku hii ni siku takatifu kwa Yawe, Mungu wenu, hivyo musiomboleze wala kulia.


Kwa muda wa yapata saa tatu, walisimama wakati Sheria ya Yawe, Mungu wao, ikisomwa. Na kwa saa tatu zilizofuata, walikuwa wakitubu na kumwabudu Yawe, Mungu wao.


Mufalme ataingia ndani watu wanapoingia, na atatoka wanapotoka.


Kisha, Yawe akanijibu hivi: Uyaandike maono haya; uyaandike wazi juu ya vibao, anayepitia pale apate kuyasoma haraka.


Kisha akawaelezea maneno yaliyoandikwa juu yake katika Maandiko Matakatifu yote, akianza toka vitabu vya Musa na kuendelea katika vitabu vya manabii wote.


Basi wakasemezana: “Mioyo yetu ilichangamuka sana wakati alipokuwa akisimulia nasi katika njia na kutuelezea Maandiko Matakatifu.”


Halafu akawafungua akili kusudi wapate kufahamu Maandiko Matakatifu


Halafu wakapanga siku ya kukutana na Paulo. Na siku ile watu wengi zaidi wakamufikia pahali alipopanga. Na tangu asubui mpaka magaribi Paulo akawaelezea mambo mengi na kutoa ushuhuda juu ya habari za Ufalme wa Mungu. Alitaka wasadiki habari za Yesu akitaja maneno ya Sheria ya Musa na ya vitabu vya manabii.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ