Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 8:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Kila siku, tangu siku ya kwanza mpaka ya mwisho, Ezra aliwasomea watu kitabu cha Sheria ya Mungu. Wakafanya sikukuu ile kwa muda wa siku saba. Na siku ya nane wakafanya mukutano mukubwa wa kufunga sikukuu, kama vile ilivyoagizwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 8:18
7 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ezra, ambaye alikuwa kuhani, akaenda na kuleta kitabu cha Sheria ya Musa mbele ya mukutano wote, wanaume na wanawake na yeyote aliyeweza kuelewa ile sheria. Siku hiyo ilikuwa ni siku ya kwanza ya mwezi wa saba.


Kisha Ezra akawasomea watu wote wanaume na wanawake na yeyote aliyeweza kuelewa Sheria ya Musa akiwa mbele ya Mulango wa Maji tangu asubui mpaka saa sita za muchana. Watu wote wakatega masikio yao na kusikiliza kwa uangalifu kitabu cha Sheria.


Kwa muda wa siku saba mutatoa sadaka Yawe anazopewa kwa moto. Siku ya nane mutakuwa na mukutano mutakatifu na kumutolea Yawe sadaka ya kuteketezwa. Mukutano huo ni mutakatifu. Siku hiyo musifanye kazi.


Kila mwaka munapaswa kufanya sikukuu hii kwa muda wa siku saba kwa heshima ya Yawe. Hili ni sharti la kufuata siku zote katika vizazi vyenu. Mutaifanya katika mwezi wa saba.


Siku ya nane mutakuwa na mukutano mutakatifu. Musifanye kazi siku hiyo.


Siku ya mwisho ya sikukuu ile iliyokuwa siku kubwa, Yesu akasimama na kusema hivi kwa sauti: “Mutu akiwa na kiu, akuje kwangu akunywe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ