Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Nehemia 8:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Watu wote waliorudi kutoka katika uhamisho wakatengeneza vibanda wakaishi ndani yake. Hii ilikuwa ni mara ya kwanza watu kuishi katika vibanda tangu wakati Yesua mwana wa Nuni alipokuwa akiishi. Watu wakafurahi sana.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Nehemia 8:17
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi siku ile wakakula na kunywa kwa furaha kubwa mbele ya Yawe. Kwa mara ya pili wakamuweka Solomono mwana wa Daudi kuwa mufalme. Wakamupakaa mafuta apate kuwa mutawala katika jina la Yawe, na Zadoki akuwe kuhani.


Kukakuwa furaha kubwa sana Yerusalema, maana tangu wakati wa mufalme Solomono mwana wa Daudi, mufalme wa Israeli jambo kama hilo lilikuwa halijatokea Yerusalema.


Pasaka kama hiyo ilikuwa haikufanyika katika Israeli yote tangu siku za nabii Samweli. Hakujatokea mufalme hata mumoja wa Israeli aliyefanya Pasaka kama hii iliyofanyika na mufalme Yosia, makuhani, Walawi na watu wote wa inchi ya Yuda, wa Israeli vilevile na wakaaji wa Yerusalema.


Alitoa sadaka zile kadiri ilivyotakiwa na amri ya Musa kila siku takatifu, ni kusema siku za Sabato, sikukuu za mwandamo wa mwezi, na sikukuu tatu za kila mwaka – sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, sikukuu ya majuma na sikukuu ya vibanda.


Wakafanya sikukuu ya vibanda kama ilivyoandikwa katika Sheria; kila siku walitoa sadaka za kuteketezwa kwa moto zilizohitajika kwa ajili ya siku hiyo.


Neno alifanywa kuwa mutu, naye akaishi kati yetu, akijaa neema na ukweli. Tuliona utukufu wake, utukufu ule Mwana wa pekee aliopewa na Baba.


Kwa siku saba mutamufanyia Yawe, Mungu wenu, karamu pahali ambapo Yawe atachagua; kwa sababu Yawe, Mungu wenu atawabariki kwa mazao yenu yote na katika shuguli zenu zote nanyi hakika mutafurahi.


Watu hawa wote walikufa katika imani pasipo kupokea mambo Mungu aliyoahidi. Lakini waliyaona kwa mbali na kuyafurahia, wakikubali kwamba walikuwa wageni na wasafiri katika dunia.


Kwa njia ya imani, aliishi kama vile mugeni katika inchi ile Mungu aliyomwahidi. Yeye alikuwa akiishi katika hema kama vile Isaka na Yakobo walivyoishi. Wao vilevile walishiriki pamoja naye ahadi ile ile ya Mungu.


Kwa maana kama Yoshua angekuwa amewafikisha watu kwenye mapumziko, Mungu hangesema tena nyuma ya pale juu ya siku ingine.


Nyuma ya kifo cha Musa mutumishi wa Yawe, Yawe alimwambia Yoshua mwana wa Nuni, musaidizi wa Musa:


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ